Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu

Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Hai lenye namba za usajili T523 EKM kugongana na lori lililokuwa limebeba shehena ya sukari lenye namba za usajili T406 CZS – T804 BUB katika eneo la Lugono Melala, barabara kuu ya Morogoro–Iringa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, amesema kuwa ilitokea majira ya alasiri ya Juni 12, 2025.

Kwa mujibu wa Ofisa Uhisiano wa  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro, Scolastica Ndunga hospitali hiyo imepokea miili ya marehemu tisa, ambapo kati ya miili hiyo, mitano ni ya wanaume na minne ni ya wanawake.

Amesema hospitali imepokea majeruhi 44, wakiwemo watu wazima 37 na watoto saba. Amesema majeruhi wengi wamepata mivunjiko na wanaendelea kupatiwa matibabu ya haraka chini ya uangalizi wa karibu wa wataalamu wa afya.

Ndunga ameongeza kuwa miili minne kati ya tisa tayari imetambuliwa na ndugu wa marehemu kupitia vitambulisho walivyokuwa navyo. Miili mingine bado haijatambuliwa na imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo, ikisubiri utambuzi na taratibu zaidi kutoka kwa familia husika.

spot_img

Latest articles

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...

Kweli IJP Wambura Polisi wamefanikiwa, sasa umma unataka kujua wasiojulikana

JUMATATU wiki hii Jeshi la Polisi lilikuwa na mahafali ya maofisa wa vyeo vya...

More like this

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...