Dkt. Jingu: Usawa wa Kijinsia ni kipaumbele cha Serikali

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

KATIBU Mkuu wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. John Jingu amesema Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imezingatia masuala ya Usawa wa kijinsia katika nyanja mbalimbali ikiwa juhudi za Serikali katika kuleta Usawa huo katika jamii.

Dkt. Jingu ameyasema hayo Juni 11, 2025 jijini Dodoma alipokutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Usawa wa Jinsia (UN Women), Hodan Addou kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa afua mbalimbali nchini juu ya uwezeshaji wanawake kiuchumi.

Dkt. Jingu ameeleza kwamba Serikali inaendelea na juhudi mbalimbali kuhakikisha kwamba Jamii inaamka na kuachana na ukatili wa kijinsia ambao umekua ni kikwazo cha maendeleo kwa ujumla.

“Kuna Kampeni ya Amsha Ari inayoendelea ambayo imelenga kujenga ufahamu juu ya masuala mbambali ya kimaendeleo kwa wananchi katika mikoa yote nchini ikiwemo suala zima la kuwainua wanawake kiuchumi“ amesema Dkt. Jingu.

Aidha Dkt. Jingu amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na ustawi wa Jinsia (UN Women) kwa kazi nzuri linalofanya katika kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuleta usawa wa jinsia nchini na kuwaeleza kuwa wanaweza kuongeza nguvu katika kampeni hiyo ya mageuzi ya kifikra ya “Amsha Ari” ili kuweza kukuza usawa wa kijinsia nchini.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Usawa wa Jinsia (UN Women) Hodan Addou ameahidi kuwa Shirika hilo litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupunguza na ukatili wa kijinsia na kukuza usawa wa kijinsia.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...