Dkt. Jingu: Usawa wa Kijinsia ni kipaumbele cha Serikali

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

KATIBU Mkuu wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. John Jingu amesema Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan imezingatia masuala ya Usawa wa kijinsia katika nyanja mbalimbali ikiwa juhudi za Serikali katika kuleta Usawa huo katika jamii.

Dkt. Jingu ameyasema hayo Juni 11, 2025 jijini Dodoma alipokutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Usawa wa Jinsia (UN Women), Hodan Addou kwa ajili ya kujadili utekelezaji wa afua mbalimbali nchini juu ya uwezeshaji wanawake kiuchumi.

Dkt. Jingu ameeleza kwamba Serikali inaendelea na juhudi mbalimbali kuhakikisha kwamba Jamii inaamka na kuachana na ukatili wa kijinsia ambao umekua ni kikwazo cha maendeleo kwa ujumla.

“Kuna Kampeni ya Amsha Ari inayoendelea ambayo imelenga kujenga ufahamu juu ya masuala mbambali ya kimaendeleo kwa wananchi katika mikoa yote nchini ikiwemo suala zima la kuwainua wanawake kiuchumi“ amesema Dkt. Jingu.

Aidha Dkt. Jingu amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na ustawi wa Jinsia (UN Women) kwa kazi nzuri linalofanya katika kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuleta usawa wa jinsia nchini na kuwaeleza kuwa wanaweza kuongeza nguvu katika kampeni hiyo ya mageuzi ya kifikra ya “Amsha Ari” ili kuweza kukuza usawa wa kijinsia nchini.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya Usawa wa Jinsia (UN Women) Hodan Addou ameahidi kuwa Shirika hilo litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika kupunguza na ukatili wa kijinsia na kukuza usawa wa kijinsia.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...