Rais Mwinyi akaribisha   wawekezaji Wachina  kuendeleza tafiti za dawa   za asili

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewakaribisha wawekezaji kutoka China kuwekeza nchini hususan kuendeleza sekta ya afya na tafiti za dawa za asili nchini.

Rais Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na timu ya wataalamu kutoka Chuo cha Utafiti wa Dawa za Asili cha China waliofika Ikulu kuonana naye.

Aidha amesema Zanzibar imeendelea kuthamini mchango na misaada ya China kwa Zanzibar katika sekta tofauti za maendeleo na kijamii iliyodumu kwa muda mrefu tangu na baada ya Mapinduzi na kuendelea hadi sasa.

Halikadhalika, ameeleza kufarijika na misaada katika sekta ya sfya inayotolewa na timu za madaktari bingwa wanaokuja nchini kwa nyakati tofauti kutoa matibabu kwa Jamii, dawa na huduma katika Hospitali na vituo vya afya na mafunzo kwa watendaji wa sekta ya afya nchini.

Naye kiongozi wa ujumbe huo Naibu Mkurugenzi wa Chuo cha Utafiti wa Dawa za Asili cha China, Professa Song Li Jwan amesema ziara yao Zanzibar imelenga kuimarisha ushirikiano baina ya China na Zanzibar hususan katika maendeleo ya sekta ya afya na kuendeleza tafiti za dawa za asili baina ya pande hizo mbili.

Amebainisha kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa sera ya kitaifa ya China kwa nchi za Afrika ikiwa ni utekelezaji wa Malengo ya Mkutano wa Beijing wa mwaka 2024 uliojikita katika uimarishaji wa Sekta ya Afya.

spot_img

Latest articles

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...

Ndege ya Air India yaanguka, ikiwa na abiria  242

Na Mwandishi Wetu Ndege ya abiria ya Shirika la Ndege la  India ‘Air India’  iliyokuwa inatokea nchini...

More like this

Wizara ya Elimu yazindua kituo cha huduma kwa wateja

Na Mwandishi Wetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imezindua Kituo cha Huduma kwa wateja,...

Watanzania  wako tayari kuchangia  harusi, sio gharama za matibabu ya mtoto- Dk. Mollel

Na Mwandishi Wetu Serikali imetoa wito kwa wananchi kubadilika na kuwekeza katika bima ya afya...

Watu tisa wafariki dunia, 44 wajeruhiwa ajali ya basi na Lori Morogoro

Na Mwandishi Wetu Watu tisa wamefariki dunia papo hapo na wengine 44 kujeruhiwa baada ya...