Rais Mwinyi akaribisha   wawekezaji Wachina  kuendeleza tafiti za dawa   za asili

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewakaribisha wawekezaji kutoka China kuwekeza nchini hususan kuendeleza sekta ya afya na tafiti za dawa za asili nchini.

Rais Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na timu ya wataalamu kutoka Chuo cha Utafiti wa Dawa za Asili cha China waliofika Ikulu kuonana naye.

Aidha amesema Zanzibar imeendelea kuthamini mchango na misaada ya China kwa Zanzibar katika sekta tofauti za maendeleo na kijamii iliyodumu kwa muda mrefu tangu na baada ya Mapinduzi na kuendelea hadi sasa.

Halikadhalika, ameeleza kufarijika na misaada katika sekta ya sfya inayotolewa na timu za madaktari bingwa wanaokuja nchini kwa nyakati tofauti kutoa matibabu kwa Jamii, dawa na huduma katika Hospitali na vituo vya afya na mafunzo kwa watendaji wa sekta ya afya nchini.

Naye kiongozi wa ujumbe huo Naibu Mkurugenzi wa Chuo cha Utafiti wa Dawa za Asili cha China, Professa Song Li Jwan amesema ziara yao Zanzibar imelenga kuimarisha ushirikiano baina ya China na Zanzibar hususan katika maendeleo ya sekta ya afya na kuendeleza tafiti za dawa za asili baina ya pande hizo mbili.

Amebainisha kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa sera ya kitaifa ya China kwa nchi za Afrika ikiwa ni utekelezaji wa Malengo ya Mkutano wa Beijing wa mwaka 2024 uliojikita katika uimarishaji wa Sekta ya Afya.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...