Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Masauni ameelezea mkakati wa Tanzania katika utekelezaji wa programu za Mabadiliko ya Tabianchini.

Ameleza hayo  katika mkutano wa kimkakati wa uwili (Bilateral Meeting) kati ya Tanzania na viongozi wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya (Europian Union)uliofanyika leo Mei 8, 2025 jijini Copenhagen, Denmark.

Mkutano huo umehudhiriwa na viongozi wakuu wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya akiwamo Wopke Hoekstra, Kamishna wa Mazingira wa Ulaya, Krzysztof Bolesta, ambaye ni Katibu wa Nchi Wizara ya Hali ya Hewa na Mazingira- Poland akimwakilisha Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Ulaya pamoja na Christian Stenberg, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Hali ya Hewa/ Mazingira, Nishati na Fedha.

Katika Mkutano huo  Masauni ameambatana na Mshauri wa Rais kuhusu masuala ya Mazingira na mabadiliko ya Tabianchi Dk. Richard Muyungi, Mwakilishi kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden pamoja na wataalam kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

Pamoja na masuala ya kubadilishana mawazo kuhusu vipaumbele kabla ya vikao vya Bonn na COP30, na mwelekeo wa nchi za Kiafrika ambapo Tanzania ni mwenyekiti wa Kundi la Majadiliano la Afrika (AGN).

Waziri Masauni ameeleza kuhusu vipaumbele vitatu vya Tanzania ambavyo ni kuendelea kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia njia mbalimbali vikiwamo vitu vya asili, kuweka mazingira rafiki kwa watanzania kutumia nishati safi ya kupikia hadi kufikia kiwango cha asilimia 80 ifikapo mwaka 2034  na kuzijengea uwezo Taasisi zinazoratibu masuala ya biashara ya kaboni nchini.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Umoja huo wa Ulaya kuangalia namna bora ya kuiwezesha katika masuala ya kujengea uwezo, misaada ya kifedha yenye masharti nafuu, ruzuku na teknolojia ya upimaji wa kiwango cha kaboni.

Akizungumza kwa niaba ya Rais wa sasa wa EU, Krzysztof Bolesta, ameipongeza Tanzania kwa namna ilivyochukua hatua za kuanzisha kituo cha kaboni ambacho ni cha  mfano kwa nchi za Afrika.

Aidha, ameeleza kuwa siku zote Umoja wa Ulaya umekuwa ukifanya kazi na kuongoza kwa mfano mzuri na kwa kudumisha uwazi na haki na hivyo itaendelea kuhakikisha inatenda haki ya kutimiza ahadi zake zote za ufadhili wa programu za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchini.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

Simba azidi kumkimbiza Yanga,  bado pointi 4

Na Mwandishi Wetu Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Pamba Jiji katika...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...