Mahakama yaamuru Lissu afikishwe mahakamani Mei 19, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu afikishwe mahakamani hapo Mei 19, 2025 na Mkuu wa Gereza la Ukonga.

Lissu anayekabiliwa na mashtaka matatu ya kuchapisha taarifa za uongo alishindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na hoja za upande wa Jamhuri kwamba kesi hiyo isikilizwe kwa njia ya mtandao, huku Lissu naye akigomea kushiriki kesi hiyo kwa njia ya mtandao.

Hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Hakimu Mkazi Mwandamizi, Geofrey Mhini ambaye ametupilia mbali hoja za upande wa Jamhuri uliotaka kesi hiyo isikilizwe kwa njia ya mtandao kutokana na sababu mbalimbali.

Katika uamuzi wake leo, Hakimu Mhini amekubaliana na hoja za Jopo la Mawakili wa utetezi wakiongozwa na Mpale Mpoki ya kwamba shauri hilo lilipaswa kuendeshwa wakati Mshtakiwa akiwepo mahakamani kwani zipo baadhi ya nyaraka anazotakiwa kusaini kwa sababu alitakiwa kusomewa maelezo ya awali (Ph).

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama, Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala amesema “Kile kilichofanywa na mahakama kwamba kesi hii isikilizwe kwa njia ya mtandao ni sahihi kanuni zinaruhusu lakini akaendelea kusema kwamba Mahakama hii haina Mamlaka ya kuamuru Magereza namna ya kukaa na mshtakiwa gerezani,”.

Naye Wakili Peter Kibatala, ambaye ni miongoni mwa Mawakili wanaomtetea amesema maamuzi ya Mahakama kukubaliana na mapingamizi yao na kuagiza mteja wao aletwe mahakamani kusomewa maelezo ya awali ni ya kushujaa na yanayolinda heshima ya muhimili huo wa dola

Wakili Kibatala ametoa wito pia kwa wananchi watakaohudhuria shauri hilo siku za usoni kuwa watulivu na kuhakikisha wanafuata miongozo ya Mahakama, katika maamuzi ya mapingamizi hayo.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...