Jessica: Vijana jitokezeni kujiandikisha awamu ya pili ya uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapiga Kura

KATIBU wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Jessica Mshama ametoa wito kwa vijana wa Kitanzania nchini kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mzunguko wa pili wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, unaotarajiwa kuanza Mei 1 hadi Julai 4, 2025.

Jessica ametoa wito huo Aprili 29, 2025 jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo pamoja na wito huo, Jessica ametoa onyo kali kwa watu wanaotaka kuwahadaa au kuwatumia vijana kwa misingi ya kuvuruga amani ya Tanzania.

Amesema ushiriki wa vijana katika uchaguzi ni muhimu kwa sababu kundi hilo pia lina asilimia 34.5 ya Watanzania wote kulingana na Sensa ya 2022. 

“Kila kijana mwenye umri wa miaka 18 au atakayefikisha miaka hiyo ifikapo siku ya Uchaguzi Mkuu, anatakiwa kuhakikisha amejiandikisha au ameboresha taarifa zake,” amesema.

Pia amewahimiza vijana kuchangamkia fursa za kugombea uongozi na kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu.

“Tanzania ya sasa inahitaji viongozi vijana wenye maono, uadilifu na uzalendo wa dhati,” amesisitiza.

Aidha Jessica ameeleza kuwa serikali chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kutengeneza zaidi ya ajira milioni nane kupitia sekta za umma na binafsi, sawa na asilimia 115 ya matarajio, kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Amefafanua miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Reli ya Kisasa ya SGR, Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, pamoja na ajira katika sekta za elimu na afya.

“Zaidi ya Sh. Bilioni 250 zimetolewa kwa makundi ya vijana kupitia mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya kuwawezesha kiuchumi,” amesema.

Jessica pia ameeleza mafanikio mengine ya serikali ikiwemo ongezeko la upatikanaji wa huduma ya maji vijijini kwa asilimia 77 na mijini kwa asilimia 88. 

Ametaja pia ujenzi wa shule mpya 3,631 za msingi na sekondari, madarasa 21,912, vituo vya afya 367 na zahanati 980.

Kwa mujibu wa Jessica, vifo vya wajawazito vimepungua kutoka 556 hadi 104 kwa kila vizazi hai 100,000 huku matumizi ya nishati safi ya kupikia yakiimarika kwa asilimia 85. Pia, huduma ya bima ya afya imeboreshwa na kuwafanya wananchi kupata matibabu kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa.

“Kuna watu wanabeza kwamba hakuna kulichofanyika, hawaoni haya yote yanayofanywa na Rais wetu Samia Suluhu Hassan. Kwahiyo niwaombe vijana wenzangu msiwasikilize watu hawa kwani hawana mapenzi mema na Nchi yetu na wanataka kuvuruga amani iliyopo,” amesisitiza Jessica.

spot_img

Latest articles

Mlugu Mtanzania wa kwanza kutinga robo fainali mashindano ya Judo Jumuiya ya Madola 2026

Glasgow, Scotland Mchezaji wa Judu, Andrew Mlugu, ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kutinga...

FURSA ZA BIASHARA ZA MABILIONI KATIKA MIGODI ZAWAFUNGUKIA WATANZANIA

Vijana na wanawake wapewa kipaumbele kunufaika na mnyororo wa thamani wa madini Na Mwandishi Wetu...

GST yaongeza kasi ya tafiti za kijiosayansi kuvutia uwekezaji sekta ya madini

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeongeza kasi ya...

UDSM wabuni mfumo wa simu janja unaosaidia wakulima kutumia maji kwa ufanisi

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaotumia...

More like this

Mlugu Mtanzania wa kwanza kutinga robo fainali mashindano ya Judo Jumuiya ya Madola 2026

Glasgow, Scotland Mchezaji wa Judu, Andrew Mlugu, ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kutinga...

FURSA ZA BIASHARA ZA MABILIONI KATIKA MIGODI ZAWAFUNGUKIA WATANZANIA

Vijana na wanawake wapewa kipaumbele kunufaika na mnyororo wa thamani wa madini Na Mwandishi Wetu...

GST yaongeza kasi ya tafiti za kijiosayansi kuvutia uwekezaji sekta ya madini

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeongeza kasi ya...