Sh. Bilioni 30 zaidhinishwa kujenga Barabara zilizoathiriwa na mvua

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kutumia kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ukarabati wa barabara muhimu za maeneo mbalimbali nchini zilizoharibiwa na mvua.

Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, ametoa taarifa hiyo mkoani Morogoro alipokwenda kwa dharura baada ya mvua kubwa zinazoendelea kunyesha kuharibu barabara inayounganisha Ifakara – Mlimba kwenda mkoa wa Njombe.

Ulega alisema pamoja na kiasi hicho cha fedha kilichoidhinishwa na Rais kwa ajili ya ujenzi wa dharura, mipango ya serikali ya ujenzi wa kudumu wa barabara na madaraja inaendelea kama ilivyo na haiathiriwi na mipango hii ya dharura.

“Nimekuja kwenu wananchi wa Morogoro – na hasa nyinyi wa Ifakara, Malinyi, Ulanga na Mlimba, kuwafikishia salamu za Rais wenu na pole zake kwa taabu hii mliyoipata. Lakini nimekuja pia na habari njema.

“Rais wenu, Samia Suluhu Hassan, amekubali matumizi ya zaidi ya shilingi bilioni 30 kwa ajili ya ujenzi wa dharura wa barabara na madaraja yaliyoharibiwa na mvua hizi zinazoendelea, hapa kwenu na maeneo mengine ya Tanzania, ili maisha yenu yaendelee. Barabara ni uchumi. Barabara ni maisha na lazima kazi ziendelee,” alisema.

Ulega aliyelazimika kukatisha kuendelea na vikao vya Bunge vinavyoendelea mkoani Dodoma kwa ajili ya kufanya safari hiyo ya dharura, alifuatana na baadhi ya wahandisi wabobezi nchini kutoka wizarani na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ili wasimamie viwango kwenye ukarabati utakaofanyika.

Kabla ya kuzungumza na wananchi wa Ifakara na viongozi waliokuwepo kwenye eneo barabara ilikokatika, Ulega alifanya ziara kwa njia ya helikopta akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, kuona athari za mvua kwenye miundombinu ya barabara na madaraja mkoani humo.

Baadhi ya miundombinu ya Morogoro kama madaraja, itafaidika pia na mpango wa serikali wa ujenzi wa madaraja na barabara wa kudumu unaoendelea nchini baada ya miradi yake kuridhiwa na serikali ya Rais Samia.

Baadhi ya barabara za Morogoro zitakazofaidika na mpango huu wa serikali ni Ulanga – Namhanga ambayo imetengewa zaidi ya shilingi bilioni 6.3 na Malinyi mpaka Mto Fulua iliyotengewa shilingi bilioni 12.

Katika taarifa yake kwa Waziri, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima alisema mkoa wa huo ni mkubwa na maombi yao kwa serikali ni kwamba barabara muhimu zijengwe katika hali ambayo zitaweza kupitika wakati wote.

spot_img

Latest articles

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

More like this

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...