Gavana Tutuba afanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa IFC, John Gandolfo

Na Mwandishi Wetu

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Tutuba, amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Taasisi ya Fedha ya Kimataifa ya Benki ya Dunia (IFC), John Gandolfo, katika ukumbi wa mikutano wa Ubalozi wa Tanzania, jijini Washington D.C., Marekani.

Katika mazungumzo hayo, walijadili masuala mbalimbali yanayohusu namna ya kuongeza upatikanaji wa mitaji na mikopo kwa sekta binafsi, ufanisi na maendeleo ya masoko ya fedha na mitaji, pamoja na fursa za uwekezaji nchini Tanzania.

Gavana Tutuba alieleza kuwa uchumi wa Tanzania ni imara na thabiti, jambo linalodhihirishwa na viashiria mbalimbali vya kiuchumi.

Alitoa wito kwa IFC pamoja na mashirika mengine ya kimataifa kuwawezesha kifedha wawekezaji wote wenye nia ya kuwekeza nchini Tanzania.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Naibu Gavana, Dkt. Yamungu Kayandabila, Mkurugenzi wa Utafiti na Sera za Uchumi BoT, Dkt. Suleiman Missango, Meneja wa Sera ya Fedha BoT, Asimwe Bashagi, pamoja na maafisa waandamizi kutoka IFC.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...