Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco afariki dunia kwa ajali

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Usambazaji Umeme Tanzania (TANESCO) Gissima Nyamo-Hanga amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo Aprili 13, 2025 kwa ajali iliyotokea Wilayani Bunda mkoani Mara.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Evansi Mtambi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo amefafanua kuwa tukio limetokea kati ya saa 6 hadi 7 usiku wa kuamkia leo.

“Ni kweli tukio lipo na Gissima amefariki Dunia na RPC atakuwa na taarifa kwa kina,” amesema Mtambi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akiahidia kutoa taarifa kwa kina badae kidogo.

Naye Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mara Nicksoni Babu amebainisha kuwa Mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule Wilaya ya Bunda huku wakisubiria taarifa zaidi na taratibu nyingine.

Media Brains inatoa pole kwa Menejimeti ya Tanesco ndugu, jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha kumpoteza mpendwa wao.

spot_img

Latest articles

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

More like this

Uwekezaji wa Shilingi Bilioni 50 Kituo Cha Mpomvu waimarisha upatikanaji wa umeme Kanda ya Ziwa

📌 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yakagua Kituo cha Kupokea...

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini yaipongeza Tanesco utekelezaji wa Mradi wa Umeme Jua Kishapu

📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake 📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi 📌 Watoa rai...

CRDB YAZINDUA KAMPENI YA ‘FAINALI NDIO MPANGO NA TEMBOCARD VISA’

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imezindua kampeni yake mpya ya 'Fainali ndio Mpango...