Dkt. Biteko: Ufundi Stadi umepewa kipaumbele na serikali

📌 Asisitiza kuwa, Rais Samia anajenga vyuo kila wilaya nchini

📌 Apongeza utoaji wa mafunzo na ujuzi kuendana na teknolojia ya kisasa

📌 Makundi maalumu kupewa kipaumbele

📌 Asema VETA itakuwa msingi kwa malezi ya watoto na Vijana

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeamua kuwekeza kwenye ufundi ili Watanzania waweze kujikomboa katika uchumi.

Hayo yamebainishwa leo Machi 21, 2025 jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA).

Dkt. Biteko amesema kuwa, Serikali imeweka msukumo mkubwa katika ufundi stadi ili Watanzania wapate elimu yenye viwango vikubwa na ujuzi wa kuweza kujikomboa katika nyanja za kiuchumi na kijamii.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anajenga VETA kila wilaya ili kuwapa ujuzi watanzania waweze kuajirika katika sekta zote,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Aidha, ameipongeza VETA kwa maadhimisho hayo kwani ni hatua kubwa na kuwataka kuendelea kufanya kazi ili kuwajengea uwezo watanzania katika ujuzi mbalimbali.

“Kwa mara myingine nawapongeza VETA kwa kuendelea kutoa mafunzo na ujuzi kuendana na mabadiliko ya teknolojia ili kuhakikisha kuwa ujuzi unatolewa kwa kuzingatia ubora na viwango vya kimataifa, ” amesema Dkt. Biteko.

Vile vile, amesisitiza elimu kutolewa kwa watu wenye mahitaji maalumu na wanaotoka kwenye mazingira magumu nchini yaweze kuongeza fursa kwa kila mtanzania kupata elimu ya ujuzi.

Naye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema kwamba, Maadhimisho ya Miaka 30 ya VETA ni uhalisia kuwa Serikali imeipa kipaumbele VETA ili vijana wapate elimu ikiwemo kujenga vyuo vya ufundi katika maeneno mengi nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa VETA, CPA, Anthony Kasore amesema kuwa, VETA imezingatia viwango na ubora wa mafunzo unazingatiwa ili vijana wanaohitimu waweze kumudu soko la ajira.

Aidha amemshukuru Rais Samia kwa usimamizi na uwezeshaji wake mkubwa katika mafunzo ya ufundi stadi nchini ili vijana waweze kupata maarifa na ujuzi ya kufanya shughuli za kiuchumi kwa tija.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...