TUJIEPUSHE KUIGA TABIA ZA KIGENI ZISIZOKUWA NA MAADILI KWA TAIFA-MAJALIWA

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema jamii inahitaji kufundishwa, kutambua na kuenzi mila za Kitanzania, pamoja na kujiepusha na vishawishi vya kuiga tabia za kigeni ambazo hazina manufaa kwa ustawi wa Taifa.

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Machi 19, 2025 katika Jubilei ya Miaka 25 ya Uaskofu wa Askofu Msaidizi Mstaafu wa Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki Bukoba Askofu Method Kilaini.

“Sote tumekua tukishuhudia ongezeko la vitendo vya ukosefu wa maadili katika jamii. Vitendo hivi vinatokana na malezi hafifu lakini pia watu kuiga mila na desturi kutoka mataifa mengine ambazo haziendani na tamaduni na maadili yetu ya Kitanzania,” amesema.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpongeza Askofu Msaidizi Mstaafu, Method Kilaini katika Jubilei ya Miaka 25 ya Uaskofu wa Askofu Msaidizi Mstaafu Method Kilaini kwenye Kanisa Kuu la Jimbo Katoliki la Bukoba, Machi 19, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu amesema hali hiyo imeathiri mwenendo wa jamii, hususan kwa vijana ambapo wanashuhudia mabadiliko katika misingi ya familia, jamii, na Taifa kwa ujumla. “Nitumie fursa hii kuliomba Kanisa kuendelea kuwa nguzo ya maadili bora, kwa kutoa mwongozo wa kiroho na kijamii,”

Amesema Kanisa lina nafasi ya pekee katika kuhakikisha Taifa linarudisha maadili ya kweli ya Kitanzania yanayofundisha kuheshimu utu, haki na amani.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo (kulia) na Askofu Msaidizi Mstaafu Method Kilain katika Jubilei ya Miaka 25 ya Uaskofu wa Askofu Msaidizi Mstaafu Kilaini iliyofanyika kwenye Kanisa Kuu  la Jimbo Katoliki la Bukoba, Machi 19, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

“Serikali, tunatambua mchango mkubwa wa Kanisa katika hili na tutashirikiana nalo ili kuleta mabadiliko chanya kwa kizazi cha sasa na kijacho,” amesema.

Amesema kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wa madhebu ya dini ikiwemo Kanisa Katoliki katika kuboresha ustawi wa jamii yetu, hivyo amewaomba viongozi wa dini nchini waendelee kuwa nguzo ya maadili bora, kwa kutoa mwongozo wa kiroho na kijamii.

Akizungumza kuhusu Askofu Kilaini, amesema ni kielelezo cha ujasiri, imani thabiti, na huduma ya kujitolea kwa Kanisa na jamii ya Watanzania, ameonesha nguvu ya uvumilivu, akiwa na michango mikubwa katika maisha ya kanisa.

spot_img

Latest articles

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

More like this

MC Pilipili afariki dunia

Na Mwandishi Wetu Mchekeshaji na mshereheshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias 'MC Pilipili' amefariki dunia leo,...

Watahiniwa 595,816 kuanza Mtihani wa Kidato cha Nne kesho

Na Tatu Mohamed JUMLA ya watahiniwa 595,816 wamesajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2025...

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...