DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

Akifungua kikao hicho katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Wilayani Kibaha, Nickson amewapongeza wajumbe wa baraza hilo kwa kazi nzuri wanayoifanya inayopelekea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Nickson amesema uhalali wa Serikali kuendelea kuwepo ni Wananchi kupata huduma za msingi, hivyo DAWASA wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya Majisafi na Majitaka ili serikali iendelee kuwepo.

Amesema maji yanaweza kuleta amani au yanaweza kuleta machafuko, hivyo maji ni muhimu, na wanachotaka wananchi wakiomba kuunganishiwa maji, waunganishiwe kwa haraka na maji yatoke kwenye bomba.

Amesema DAWASA imeiheshimisha sana Mkoa wa Pwani kwani wawekezaji wanapokuja kutaka kuwekeza tunawaambia huduma ya maji ipo ya kutosha.

“Wawekezaji wakija Pwani sisi tunawaambia tuna uhakika wa maji na hiyo inaongeza uwekezaji katika sekta ya viwanda katika mkoa wetu, sisi kufanya vizuri Mkoa wa Pwani kunatokana na uwepo wa maji ya kutosha kutoka DAWASA,” amesema Nickson.

Mkuu huyo wa Wilaya ameitaka DAWASA kuongeza kasi na juhudi katika kutoa huduma kwa wananchi ili kufikia malengo yao na kuhakikisha wananachi wanapata huduma bora wakati wote.

“Nawaomba DAWASA muongeze speed katika kutoa huduma, kuhakikisha mnadhibiti upotevu wa maji. Wananchi wa wilaya yangu, wao wanafurahia huduma za DAWASA hivyo nawapongeza sana,” amesema.

spot_img

Latest articles

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

More like this

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...