DC Kibaha afungua Baraza Kuu la Wafanyakazi DAWASA

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Kibaha, Nickson Simon amefungua kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).

Akifungua kikao hicho katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Wilayani Kibaha, Nickson amewapongeza wajumbe wa baraza hilo kwa kazi nzuri wanayoifanya inayopelekea kutoa huduma bora kwa wananchi.

Nickson amesema uhalali wa Serikali kuendelea kuwepo ni Wananchi kupata huduma za msingi, hivyo DAWASA wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya Majisafi na Majitaka ili serikali iendelee kuwepo.

Amesema maji yanaweza kuleta amani au yanaweza kuleta machafuko, hivyo maji ni muhimu, na wanachotaka wananchi wakiomba kuunganishiwa maji, waunganishiwe kwa haraka na maji yatoke kwenye bomba.

Amesema DAWASA imeiheshimisha sana Mkoa wa Pwani kwani wawekezaji wanapokuja kutaka kuwekeza tunawaambia huduma ya maji ipo ya kutosha.

“Wawekezaji wakija Pwani sisi tunawaambia tuna uhakika wa maji na hiyo inaongeza uwekezaji katika sekta ya viwanda katika mkoa wetu, sisi kufanya vizuri Mkoa wa Pwani kunatokana na uwepo wa maji ya kutosha kutoka DAWASA,” amesema Nickson.

Mkuu huyo wa Wilaya ameitaka DAWASA kuongeza kasi na juhudi katika kutoa huduma kwa wananchi ili kufikia malengo yao na kuhakikisha wananachi wanapata huduma bora wakati wote.

“Nawaomba DAWASA muongeze speed katika kutoa huduma, kuhakikisha mnadhibiti upotevu wa maji. Wananchi wa wilaya yangu, wao wanafurahia huduma za DAWASA hivyo nawapongeza sana,” amesema.

spot_img

Latest articles

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...

Tanzania yataka ushirikiano imara na kuvuka mipaka kutokomeza maralia 

Na John Mapepele, Geneva, Uswisi  WAZIRI wa Afya wa Tanzania, Mohamed Mchengerwa, ametoa wito wa...

More like this

Tanesco yaendelea kuwaelimisha wanaofanya shughuli za kiuchumi kwenye miundombinu ya umeme

📌Ni katika muendelezo wa ukaguzi wa miundombinu ya umeme Dar es salaam 📌Yatoa rai kwa...

‎DAWASA yapeleka agenda ya kudhibiti upotevu wa maji Pwani

Na Mwandishi Wetu MAPAMBANO dhidi ya upotevu wa maji yamepokelewa vyema na uongozi wa...

Msaidizi wa Lissu apatikana na pingu mkononi, aeleza kilichomkuta

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, Amani...