Benki ya Stanbic kuendelea kuzisaidia Kampuni ndogo za uchimbaji wa mafuta na gesi

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya Stanbic imesema kuwa itaendelea kushirikiana na makampuni madogo ya Kitanzania yanayojishughulisha na uchimbaji wa mafuta na gesi katika kuwapa uzoefu katika miradi mikubwa ijayo.

Hayo yameelezwa leo Machi 06, 2025 na Makamu wa Rais wa Miundombinu ya Nishati, Joe Mwakenjuki katika Kongamano na maonesho ya Petroli ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) amesema wameona makampuni ya watanzania yakijitokeza katika kuangalia fursa mbalimbali katika miradi ya mafuta na gesi.

Amesema Benki ya Stanbic imeweza kusaidia makampuni hayo madogo ya kizalendo katika mnyororo wa thamani kwenye shughuli zao za mafuta na gesi.

“Benki yetu imekuwa mstari wa mbele katika kusaidia Kampuni ndogo za kitanzania katika kuwapa uzoefu katika miradi yao ya sasa wanayofanya ambayo ni midogo. Ni vema wenyewe kujipa uzoefu katika miradi ya sasa na sio kusubiri miradi mikubwa ya mafuta na gesi kufanya hata hii midogo wanaweza kufanya,” amesema Mwakenjuki.

Amefafanua kuwa Watanzania wanaendelea kujitokeza kwa wingi katika kuchangamkia fursa za miradi ya mafuta na gesi na kujiandaa na miradi mikubwa zaidi kuliko wanayotekelezwa kwa sasa.”Wanaweza kuja katika mabenki na kuweza kuwasaidia kupata uzoefu ili miradi mikubwa inapokuja tutaweza kuwasaidia zaidi kwani mahitaji ya kifedha,” amesema.

Amefafanua kuwa Stanbic Bank inashiriki kikamilifu katika kufadhili sekta ya mafuta na gesi barani Afrika kwa kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa njia endelevu na inatoa huduma za kifedha kama mikopo, biashara ya kifedha, na ushauri kwa kampuni zinazojihusisha na mafuta na gesi.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Kilo 101.2 za Mirungi ndani ya Basi la Abood, watano mbaroni

Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata...

Wakurugenzi Media Brains waapishwa kuwa Majaji tuzo za EJAT

Na Mwandishi Wetu WAKURUGENZI wa Kampuni ya Media Brains wameapishwa wameteuliwa na Baraza la Habari...

CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya...

Mchezaji auawa na majambazi nchini Ghana

MCHEZAJI wa soka nchini Ghana, Dominic Frimpong, ameuawa kwa kupigwa risasi baada ya...

More like this

DCEA yakamata Kilo 101.2 za Mirungi ndani ya Basi la Abood, watano mbaroni

Na Mwandishi wetu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata...

Wakurugenzi Media Brains waapishwa kuwa Majaji tuzo za EJAT

Na Mwandishi Wetu WAKURUGENZI wa Kampuni ya Media Brains wameapishwa wameteuliwa na Baraza la Habari...

CRDB yaandika historia, yapata faida ya Trilioni 1

Na Mwandishi wetu BENKI ya CRDB imepata faida ya Sh trilioni moja kabla ya...