Rais Samia: Ujenzi Kituo cha kupoza umeme Handeni kuimarisha upatikanaji umeme

📌 Kituo kugharimu shilingi bilioni 50

📌 Zaidi ya Shillingi billioni 98 kutekeleza mradi wa gridi imara Kilindi

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema utekelezaji wa ujenzi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Handeni mkoani Tanga utakapokamilika utaboresha upatikanaji wa umeme katika Wilaya za Handeni na Kilindi pamoja na maeneo jirani.

Rais Samia ameyasema hayo leo Februari 25, 2025 katika ziara yake mkoani Tanga wakati akizungumza na wananchi wa Handeni mara baada ya kuzindua Shule ya Wasichana ya Kilindi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.

“Tatizo la umeme hapa Handeni Serikali inalifahamu, imeanza kuchukua hatua kwa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme kitakachogharimu takribani shilingi bilioni 50 za kitanzania ambacho kitaboresha upatikanaji wa umeme,” amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa, upatikanaji wa umeme wa uhakika Handeni utasaidia ukuaji wa uchumi pamoja na kuyainua madini ya kinywe ambayo yanapatikana Wilaya ya Kilindi na yanahitaji umeme wa kutosha.

Awali, Mbunge wa Kilindi, Omari Kigua aliishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 98 kwa ajili ya kutekeleza mradi ya gridi imara utakao husisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Mkata kupitia Handeni hadi Kilindi.

Kigua ameeleza kuwa Wilaya ya Kilindi ina Vijiji 102 ambavyo vyote vimefikiwa na umeme na sasa kazi inayoendelea ni ya kufikisha umeme kwenye Vitongoji.

spot_img

Latest articles

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...

Tuzo za TFF za msimu wa 2024/25 zayeyuka

Na Mwandishi Wetu Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa taarifa ya kuahirisha hafla ya utoaji...

More like this

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

Uwanja wa Mkwakwani wafungiwa

Na Mwandishi Wetu SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limeufungia Uwanja wa Mkwakwani, Tanga kutumika kwa...