RAIS SAMIA: NAMRUDISHA MWANANGU JANUARI KWA MAMA, NILIMPIGA KOFI

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amesema  anamrudisha Januari Makamba kwa mama kwani alimpiga kofi na kumfichia chakula  kama ilivyo desturi ya kina mama pindi mtoto anapomkera.

Rais Samia amezungumza hayo  leo Februari 24,2025 wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Lushoto mkoani, Tanga.

“Nataka nimuite mwanangu Januari hapa aje huku,arudi kwa mama, Sisi wamama mnatujua, ukimkera mama anakupiga kikofi, anakufichia chakula. Sasa mwanangu nilimpiga kikofi  na kumfichia chakula, lakini leo namrudisha kwa mama. Haya mwanangu njoo,” amesema Rais Samia huku akimkumbatia Makamba.

Katika hatua nyingine Rais Samia amezindua jengo la Halmashauri ya Bumbuli, wilayani humo na kusema kuwa madhumuni ya jengo hilo ni kusogeza huduma karibu ambapo na wananchi ambapo huduma zote zitakuwa zinapatikana humo.

spot_img

Latest articles

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

More like this

Kamati ya kudumu ya Binge Nishati na Madini yaridhishwa na maendeleo ya Kiwanda cha nguzo za zege

📌Ni mradi wa kihistoria kutekelezwa chini ya Serikali ya awamu ya Sita 📌 Yaipongeza...

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...