RAIS SAMIA: NAMRUDISHA MWANANGU JANUARI KWA MAMA, NILIMPIGA KOFI

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan amesema  anamrudisha Januari Makamba kwa mama kwani alimpiga kofi na kumfichia chakula  kama ilivyo desturi ya kina mama pindi mtoto anapomkera.

Rais Samia amezungumza hayo  leo Februari 24,2025 wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Lushoto mkoani, Tanga.

“Nataka nimuite mwanangu Januari hapa aje huku,arudi kwa mama, Sisi wamama mnatujua, ukimkera mama anakupiga kikofi, anakufichia chakula. Sasa mwanangu nilimpiga kikofi  na kumfichia chakula, lakini leo namrudisha kwa mama. Haya mwanangu njoo,” amesema Rais Samia huku akimkumbatia Makamba.

Katika hatua nyingine Rais Samia amezindua jengo la Halmashauri ya Bumbuli, wilayani humo na kusema kuwa madhumuni ya jengo hilo ni kusogeza huduma karibu ambapo na wananchi ambapo huduma zote zitakuwa zinapatikana humo.

spot_img

Latest articles

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

More like this

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...