JANUARI MAKAMBA AMSHUKURU RAIS SAMIA KUMFUNZA MENGI

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga Januari Makamba, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini na kumteua  kuwa Waziri wa Nishati na Mambo ya Nje na kusema jambo hilo litaendelea kuwa historia isiyofutika katika maisha yake.

Akizungumza leo Februari 24,2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Sabasaba, Wilaya ya Lushoto, Tanga, Makamba amesema amejifunza mengi kupitia uongozi wa Rais Samia ameerevuka.

“Mheshimiwa Rais, naomba nikushukuru sana kutoka sakafu ya moyo wangu kwa kuniamini mimi kuniteua waziri wako, kwanza wa nishati na baadaye Mambo ya Nje ni heshima kubwa ambayo haitafutika katika uhai wa maisha yangu.

“Katika kipindi ambacho nimefanya kazi na wewe nimejifunza sana na nimeerevuka kutokana na uongozi wako. Lakini nimeerevuka sana kutokana na Uongozi wako. Lakini kabla ya hapo Mheshimiwa Rais  utakumbuka mimi nilikuwa Waziri wa Nchi chini ya Ofisi yako, tumefanya kazi wote miaka minne na ilikuwa ndiyo nafasi yangu ya kwanza kuwa Waziri, Wewe ndiyo umenifundisha kuwa Waziri, kwa hiyo kama kuna werevu nilionao basi unatokana na mikono yako na hii nitakwenda nayo kaburini kwangu,” amesema Makamba.

spot_img

Latest articles

RC Chalamila tafuta dozi ya Tume Keenja

KATIKA juhudi za kurejesha utawala wa sheria (orderly administration) katika jiji la Dar es...

DAWASA YAANZA MSAKO KWA WANAOJIUNGANISHIA MAJI KINYEMELA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)...

Vipengele 63 Kuing’arisha The Serengeti Awards 2026

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya vipengele 63 vitaingia katika kinyang’anyiro cha The Serengeti Awards...

PSSSF yawajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu masuala ya Hifadhi ya Jamii

Dar es Salaam- Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeendesha...

More like this

RC Chalamila tafuta dozi ya Tume Keenja

KATIKA juhudi za kurejesha utawala wa sheria (orderly administration) katika jiji la Dar es...

DAWASA YAANZA MSAKO KWA WANAOJIUNGANISHIA MAJI KINYEMELA

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA)...

Vipengele 63 Kuing’arisha The Serengeti Awards 2026

Na Mwandishi Wetu JUMLA ya vipengele 63 vitaingia katika kinyang’anyiro cha The Serengeti Awards...