JANUARI MAKAMBA AMSHUKURU RAIS SAMIA KUMFUNZA MENGI

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga Januari Makamba, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini na kumteua  kuwa Waziri wa Nishati na Mambo ya Nje na kusema jambo hilo litaendelea kuwa historia isiyofutika katika maisha yake.

Akizungumza leo Februari 24,2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Sabasaba, Wilaya ya Lushoto, Tanga, Makamba amesema amejifunza mengi kupitia uongozi wa Rais Samia ameerevuka.

“Mheshimiwa Rais, naomba nikushukuru sana kutoka sakafu ya moyo wangu kwa kuniamini mimi kuniteua waziri wako, kwanza wa nishati na baadaye Mambo ya Nje ni heshima kubwa ambayo haitafutika katika uhai wa maisha yangu.

“Katika kipindi ambacho nimefanya kazi na wewe nimejifunza sana na nimeerevuka kutokana na uongozi wako. Lakini nimeerevuka sana kutokana na Uongozi wako. Lakini kabla ya hapo Mheshimiwa Rais  utakumbuka mimi nilikuwa Waziri wa Nchi chini ya Ofisi yako, tumefanya kazi wote miaka minne na ilikuwa ndiyo nafasi yangu ya kwanza kuwa Waziri, Wewe ndiyo umenifundisha kuwa Waziri, kwa hiyo kama kuna werevu nilionao basi unatokana na mikono yako na hii nitakwenda nayo kaburini kwangu,” amesema Makamba.

spot_img

Latest articles

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Mradi wa Taza kufungua Soko jipya la biashara ya umeme Afrika

Na Mwandishi Wetu, Mbeya IMEELEZWA kuwa mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya...

More like this

Viongozi wa dini Kanda ya Magharibi waazimia kudumisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Tabora VIONGOZI wa dini katika mikoa ya Kanda ya Magharibi wameazimia...

Viongozi wa Dini Kanda ya Kusini wataka ulinzi amani, kujitokeza upigaji kura

Na Mwandishi Wetu, Lindi VIONGOZI wa dini mbalimbali kutoka mikoa ya Kanda ya Kusini wamewataka...

Lissu anyimwa dhamana, kesi yaahirishwa hadi Nov 3

Na Mwandishi Wetu Kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...