JANUARI MAKAMBA AMSHUKURU RAIS SAMIA KUMFUNZA MENGI

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga Januari Makamba, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini na kumteua  kuwa Waziri wa Nishati na Mambo ya Nje na kusema jambo hilo litaendelea kuwa historia isiyofutika katika maisha yake.

Akizungumza leo Februari 24,2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Sabasaba, Wilaya ya Lushoto, Tanga, Makamba amesema amejifunza mengi kupitia uongozi wa Rais Samia ameerevuka.

“Mheshimiwa Rais, naomba nikushukuru sana kutoka sakafu ya moyo wangu kwa kuniamini mimi kuniteua waziri wako, kwanza wa nishati na baadaye Mambo ya Nje ni heshima kubwa ambayo haitafutika katika uhai wa maisha yangu.

“Katika kipindi ambacho nimefanya kazi na wewe nimejifunza sana na nimeerevuka kutokana na uongozi wako. Lakini nimeerevuka sana kutokana na Uongozi wako. Lakini kabla ya hapo Mheshimiwa Rais  utakumbuka mimi nilikuwa Waziri wa Nchi chini ya Ofisi yako, tumefanya kazi wote miaka minne na ilikuwa ndiyo nafasi yangu ya kwanza kuwa Waziri, Wewe ndiyo umenifundisha kuwa Waziri, kwa hiyo kama kuna werevu nilionao basi unatokana na mikono yako na hii nitakwenda nayo kaburini kwangu,” amesema Makamba.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...