JANUARI MAKAMBA AMSHUKURU RAIS SAMIA KUMFUNZA MENGI

Na Mwandishi Wetu

MBUNGE wa jimbo la Bumbuli Mkoani Tanga Januari Makamba, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kumuamini na kumteua  kuwa Waziri wa Nishati na Mambo ya Nje na kusema jambo hilo litaendelea kuwa historia isiyofutika katika maisha yake.

Akizungumza leo Februari 24,2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Sabasaba, Wilaya ya Lushoto, Tanga, Makamba amesema amejifunza mengi kupitia uongozi wa Rais Samia ameerevuka.

“Mheshimiwa Rais, naomba nikushukuru sana kutoka sakafu ya moyo wangu kwa kuniamini mimi kuniteua waziri wako, kwanza wa nishati na baadaye Mambo ya Nje ni heshima kubwa ambayo haitafutika katika uhai wa maisha yangu.

“Katika kipindi ambacho nimefanya kazi na wewe nimejifunza sana na nimeerevuka kutokana na uongozi wako. Lakini nimeerevuka sana kutokana na Uongozi wako. Lakini kabla ya hapo Mheshimiwa Rais  utakumbuka mimi nilikuwa Waziri wa Nchi chini ya Ofisi yako, tumefanya kazi wote miaka minne na ilikuwa ndiyo nafasi yangu ya kwanza kuwa Waziri, Wewe ndiyo umenifundisha kuwa Waziri, kwa hiyo kama kuna werevu nilionao basi unatokana na mikono yako na hii nitakwenda nayo kaburini kwangu,” amesema Makamba.

spot_img

Latest articles

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

More like this

Natoa nishani ya uthubutu kwa Kanisa Katoliki 2025

Siyo hulka yangu kujadili masuala ya dini katika chambuzi ninazofanya. Wala, sikusudii kujikita kuibua...

Benki ya CRDB yafunga mwaka kwa kukabidhi zawadi ya magari kwa washindi wa Simbanking

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB, imemkabidhi Deo Ferdinand Mlawa na wenzake watano zawadi...

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...