BAADHI YA MAENEO DAR, PWANI, ZNZ KUKOSA UMEME FEB 22-28

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),limetoa taarifa ya uwepo wa maboresho katika kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Msongo wa Kilovoti 220 cha Ubungo kilichopo jijini Dar es Salaam kuanzia February 22- 28, 2025, hivyo baadhi ya maeneo ya Zanzibar na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani yataathirika kwa kukosa umeme kwa nyakati tofauti.

Katika taarifa ya TANESCO iliyotolewa leo February 19,2025 imesema hatua hiyo ni muhimu kwa Shirika kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja wake kufuatia ongezeko la mahitaji ya matumizi ya umeme katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Pwani ambalo limefanya kituo hicho kuzidiwa na hivyo kulazimu kufungwa kwa mashine mpya (Transformer) kubwa yenye uwezo wa MVA 300 ili kukidhi mahitaji ya umeme katika maeneo tajwa.

“Katika kipindi hicho ambacho huduma ya umeme itakosekana kwa nyakati tofauti Shirika pia litakuwa likifanya matengenezo mbalimbali ya miundombinu ya umeme kwenye maeneo tajwa ili kuiweka miundombinu yetu kenye hali ya imara hasa kwenye kipindi hiki tunachoelekea cha msimu
wa mvua.

“Shirika linaomba radhi kwa usumbufu katika kipindi chote ambacho huduma ya umeme itakosekana kwenye baadhi ya maeneo na litaendelea kutoa taarifa za maendeleo ya kazi hiyo mpaka kukamilika kwake,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Suluhisho la kusambaza taarifa za Hali ya Hewa kwa wakati kwa wakulima lajadiliwa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Norges...

Dkt. Mwigulu ataka ushirikiano wa kikanda kwenye mapambano dhidi ya saratani

▪Asisitiza Tanzania itaendelea kuwa kituo bora cha ushirikiano wa kikanda na Afrika ▪Asema shilingi bilioni...

Rais Samia hawezi kujivua uanadiplomasia akiwa ikulu

Dunia tunayoishi sasa mataifa hutegemeana. Huheshimiana na kuhitajiana. Ndiyo maana hata nchi za ulimwengu...

Msimu wa pili mbio za Pande Marathon kuzinduliwa Feb 14 Siku ya Wapendanao

Na Mwandishi Wetu UZINDUZI wa mbio za Msakuzi Pande Game Reserve Marathon awamu ya...

More like this

Suluhisho la kusambaza taarifa za Hali ya Hewa kwa wakati kwa wakulima lajadiliwa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Norges...

Dkt. Mwigulu ataka ushirikiano wa kikanda kwenye mapambano dhidi ya saratani

▪Asisitiza Tanzania itaendelea kuwa kituo bora cha ushirikiano wa kikanda na Afrika ▪Asema shilingi bilioni...

Rais Samia hawezi kujivua uanadiplomasia akiwa ikulu

Dunia tunayoishi sasa mataifa hutegemeana. Huheshimiana na kuhitajiana. Ndiyo maana hata nchi za ulimwengu...