BAADHI YA MAENEO DAR, PWANI, ZNZ KUKOSA UMEME FEB 22-28

Na Mwandishi Wetu

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),limetoa taarifa ya uwepo wa maboresho katika kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Msongo wa Kilovoti 220 cha Ubungo kilichopo jijini Dar es Salaam kuanzia February 22- 28, 2025, hivyo baadhi ya maeneo ya Zanzibar na mikoa ya Dar es Salaam na Pwani yataathirika kwa kukosa umeme kwa nyakati tofauti.

Katika taarifa ya TANESCO iliyotolewa leo February 19,2025 imesema hatua hiyo ni muhimu kwa Shirika kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja wake kufuatia ongezeko la mahitaji ya matumizi ya umeme katika maeneo ya Zanzibar, Dar es Salaam na Pwani ambalo limefanya kituo hicho kuzidiwa na hivyo kulazimu kufungwa kwa mashine mpya (Transformer) kubwa yenye uwezo wa MVA 300 ili kukidhi mahitaji ya umeme katika maeneo tajwa.

“Katika kipindi hicho ambacho huduma ya umeme itakosekana kwa nyakati tofauti Shirika pia litakuwa likifanya matengenezo mbalimbali ya miundombinu ya umeme kwenye maeneo tajwa ili kuiweka miundombinu yetu kenye hali ya imara hasa kwenye kipindi hiki tunachoelekea cha msimu
wa mvua.

“Shirika linaomba radhi kwa usumbufu katika kipindi chote ambacho huduma ya umeme itakosekana kwenye baadhi ya maeneo na litaendelea kutoa taarifa za maendeleo ya kazi hiyo mpaka kukamilika kwake,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu...

Wanariadha Wanawake 155 kukiwasha kwa Mkapa Nov 29

Na Winfrida Mtoi Jumla ya wanariadha wanawake 155, wanatarajiwa kushiriki katika msimu wa saba wa...

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

More like this

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu  ajiuzulu TEF

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejiuzulu nafasi ya makamu...

Wanariadha Wanawake 155 kukiwasha kwa Mkapa Nov 29

Na Winfrida Mtoi Jumla ya wanariadha wanawake 155, wanatarajiwa kushiriki katika msimu wa saba wa...

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...