Mkandarasi anayejenga Barabara za Tactic Morogoro atakiwa kukamilisha kazi ndani ya miezi mitatu

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila amemtaka Mkandarasi M/s Jiangxi GEO Engineering Group anayejenga barabara ya Kihonda – VETA yenye urefu wa Km 12.85 kwa kiwango cha lami Manispaa ya Morogoro mkoani Morogoro kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa ubora unaotakiwa ndani ya miezi mitatu hadi kufikia mwezi Mei 2025.

Mhandisi Mativila ametoa agizo hilo kwa mkandarasi pamoja na Mhandisi Mshauri wa mradi huo katika ziara ya ukaguzi wa mradi huo unaotekelezwa kupitia Mradi wa Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTIC) chini ya mkopo nafuu toka Benki ya Dunia.

“Nimekuja kutembelea moja ya miradi mikubwa ambayo serikali ya awamu ya sita inatekeleza kwa ajili ya kuleta maendeleo na ushindani katika miji 45 ya Tanzania iliyochanguliwa iwe na ushindani wa kuwa na miundombinu bora ikiwemo ya barabara kwa kiwango cha lami inayowezesha kukua kwa uchumi’’, amesema.

Amefafanua kuwa, kati ya miji hiyo ni pamoja na Manispaa ya Morogoro ambayo inanufaika na utekelezaji wa mradi huo mkubwa ambapo kwa mkoa huo mradi unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 19.6.

“Mradi huu umechelewa na upo nyuma kwa asilimia 18 na kwamba umetekelezwa kwa asilimia 82 tu na kuna sababu kadhaa ambazo zimeelezwa, baada ya kuweka mambo sawa tunataka mradi huu ukamilike ndani ya muda wa miezi mitatu endapo kukiwa na mvua kubwa basi mradi uwe umekamilika Agosti, mwaka huu“, amesema.

Naye, Meneja wa TARURA Wilaya ya Morogoro, Mhandisi Mohamed Muanda amesema ujenzi wa mradi huo ulianza Oktoba 23, 2024 na kutakiwa kukamilika Februari 2025 ambapo awamu ya kwanza inahusisha ujenzi wa mifereji mikubwa ya maji ya mvua kuelekea mto Kikundi yenye urefu wa jumla ya Km 4.4, ujenzi wa ofisi ya Mhandisi Mshauri na ofisi ya wasimamizi wa miradi.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mhandisi Mshauri kutoka nchini pamoja na Mhandisi Mshauri kutoka Ethiopia (JV Core consultancy), Dargie Dilbedi amemhakikishia Naibu Katibu kwamba kazi hiyo ipo katika hatua ya mwisho na kwamba anatumaini ndani ya miezi mitatu ya nyongeza itakamilika

spot_img

Latest articles

Dk. Nchimbi: Uhuru wa Mahakama situmike kuficha uzembe

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametoa rai kwa Majaji na Mahakimu...

Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda...

Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa...

Watanzania Watakiwa Kujitokeza Kuomba Nafasi 1,150 za Udereva Qatar

Na Mwandishi Wetu WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuchangamkia fursa ya ajira iliyotangazwa na...

More like this

Dk. Nchimbi: Uhuru wa Mahakama situmike kuficha uzembe

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais Dk. Emmanuel Nchimbi ametoa rai kwa Majaji na Mahakimu...

Rais Samia kushiriki mkutano wa WGS 2026

Na Mwandishi Wetu RAIS Samia Suluhu Hassan ameondoka nchini leo Februari 2, 2026 kwenda...

Yanga yaingilia ugomvi wa Mangungu na mshabiki Simba

Na Mwandishi Wetu UONGOZI wa Klabu ya Yanga umesema umesikitishwa na kitendo cha vurugu alichofanyiwa...