CCM yamfukuza aliyepinga Rais Samia kupitishwa mgombea pekee Urais

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, kimemfukuza uanachama kada wa chama hicho Mchungaji Godfrey Malisa kuanzia leo Februari 10, 2025 kwa tuhuma za kukiuka Katiba na maadili ya Chama hicho.

Hatua ya kufukuzwa kwa Malisa imeelezwa kuwa inatokana na kauli alizokuwa akizitoa kupinga uamuzi wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa wa Januari 19, 2025 akidai kupitisha kwa wagombea hao (Rais Samia Suluhu Hassan (Tanzania Bara) na Dk Hussein Mwinyi- Zanzibar) kumekiuka Katiba ya CCM.

Mchungaji Malisa, ambaye amewahi kugombea urais, uspika na hata ubunge, alijiunga na CCM mwaka 2021 na alikuwa miongoni mwa makada tisa waliochukua fomu kugombea uenyekiti wa Chama hicho mwaka 2022.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 10, 2025 Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Merce Mollel amesema uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ya mkoa.

spot_img

Latest articles

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...

Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter...

TCAA yaimarisha usalama wa anga kwa mifumo ya kisasa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imejizatiti kuendana na mabadiliko...

More like this

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...

Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter...