CCM yamfukuza aliyepinga Rais Samia kupitishwa mgombea pekee Urais

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, kimemfukuza uanachama kada wa chama hicho Mchungaji Godfrey Malisa kuanzia leo Februari 10, 2025 kwa tuhuma za kukiuka Katiba na maadili ya Chama hicho.

Hatua ya kufukuzwa kwa Malisa imeelezwa kuwa inatokana na kauli alizokuwa akizitoa kupinga uamuzi wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa wa Januari 19, 2025 akidai kupitisha kwa wagombea hao (Rais Samia Suluhu Hassan (Tanzania Bara) na Dk Hussein Mwinyi- Zanzibar) kumekiuka Katiba ya CCM.

Mchungaji Malisa, ambaye amewahi kugombea urais, uspika na hata ubunge, alijiunga na CCM mwaka 2021 na alikuwa miongoni mwa makada tisa waliochukua fomu kugombea uenyekiti wa Chama hicho mwaka 2022.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 10, 2025 Katibu wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Merce Mollel amesema uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM ya mkoa.

spot_img

Latest articles

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...

Mwanasheria Mkuu asisitiza mageuzi ya Sheria za Anga

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesisitiza juu ya umuhimu wa...

Wananchi Peramiho, Shiwinga kupiga Kura kesho kuchagua Mbunge, Diwani

Na Mwandishi Wetu WAPIGA Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura...

MIF 2026 kujadili mikakati ya kufikia uchumi wa kati wa juu 2050

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imesema Mkutano wa Jukwaa la Wakurugenzi wa Bodi na Watendaji...

More like this

Haikubaliki, hali hii ya D’Salaam inachefua

KATIKA siku za hivi karibuni kumekuwa na matamko ya operesheni mbalimbali za kurejesha uzingatiaji...

Mwanasheria Mkuu asisitiza mageuzi ya Sheria za Anga

Na Mwandishi Wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesisitiza juu ya umuhimu wa...

Wananchi Peramiho, Shiwinga kupiga Kura kesho kuchagua Mbunge, Diwani

Na Mwandishi Wetu WAPIGA Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura...