Serikali inafanyia kazi maboresho ya tozo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI kupitia Wizara ya Madini inaendelea na juhudi za kupunguza mzigo wa tozo kwa Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu hapa nchini kwa kufanya mapitio ya ada na ushuru mbalimbali unaotozwa katika mnyororo wa uchimbaji na uchenjuaji wa madini hayo.

Hatua hiyo imebainishwa na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, leo Februari 7, 2025, Bungeni Jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Busanda, Tumaini Magessa ambaye alitaka kujua ni lini Serikali itapitia upya tozo zilizopo kwenye mnyororo wa uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu zinazowaelemea Wachimbaji Wadogo.

Katika majibu yake, Waziri Mavunde amesema kuwa kupitia Mkakati wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (MKUMBI), Wizara ya Madini imefanya utafiti wa tozo 66 zinazotozwa na Halmashauri mbalimbali katika shughuli za uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu na kutaja baadhi ya tozo hizo kuwa ni ushuru wa karasha, ada ya ukaguzi, kodi ya ongezeko la thamani (VAT in leaching/CIP), ushuru wa kusafirisha miamba ya madini, na visusi (mabaki ya miamba baada ya uchenjuaji).

“Katika kutatua changamoto hizi, Wizara iliitisha kikao Mwezi Agosti, 2024 Mkoani Singida ambacho kilishirikisha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Wizara ya Fedha, Tume ya Madini, STAMICO, Halmashauri za Wilaya (Ikungi, Chunya, Kahama, Msalala, Meatu, Shinyanga, Mtama na Lindi), FEMATA na TAWOMA. Rasimu ya Mapendekezo ya Maboresho tayari imeshaandaliwa na ipo katika hatua ya kufanyiwa mapitio na tathmini, ambapo Matokeo ya tathmini hiyo yatatusaidia katika kupanga tozo rafiki kwa wachimbaji wadogo,” amesema Mavunde.

Aidha, Waziri Mavunde ameongeza kuwa, Serikali inaendelea na maboresho makubwa ya mfumo wa kodi kupitia Tume ya Maboresho ya Kodi iliyoanzishwa na Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan na kwamba tume hiyo inatarajiwa kutoa mapendekezo yatakayosaidia kupunguza changamoto za kikodi zinazowakabili Wachimbaji Wadogo wa Dhahabu na Sekta ya Madini kwa ujumla.

Hatua hizo zinadhihirisha dhamira ya Serikali katika kuboresha mazingira ya uchimbaji mdogo wa madini na kukuza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa nchi.

spot_img

Latest articles

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...

Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama...

More like this

Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao...

Serikali yaahidi kushirikiana na wadau kuendeleza mchezo wa kuogelea

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wakuogelea Afrika Mashariki wamekutana kujadili maendeleo ya mchezo huo,...

Ndejembi: Tanesco mmefanya mageuzi makubwa katika huduma ya umeme kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme Tanzania...