Vijana 331 wachaguliwa kujiunga na mafunzo idara ya uhamiaji

Na Mwandishi Wetu

IDARA ya Uhamiaji Tanzania imetangaza majina ya vijana 331 waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya idara hiyo kuanzia Machi 1, 2025.

Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo hayo limetolewa leo Alhamisi Februari 6, 2025 na Kamishna Jenerali wa idara hiyo.

“Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anawatangazia vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na Idara ya Uhamiaji kuripoti Chuo cha Uhamiaji cha Raphael Kubaga kilichopo Boma Kichakamiba, Wilaya ya Mkinga – Mkoani Tanga, Jumamosi Machi mosi 2025 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana,” imeeleza taarifa hiyo.

Pia, kwa walioomba na kuchaguliwa kupitia Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, wanatakiwa kuripoti Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Unguja (Tunguu) Jumatatu Februari 24, 2025 saa 2:00 asubuhi.

Katika taarifa hiyo vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo hayo wametakiwa kuripoti wakiwa na vyeti halisi vya elimu na fani mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

More like this

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

Livembe: Mchakato wa Uchaguzi ulikuwa wa haki na halali

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Hamis Livembe, amesema mchakato wa...

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...