Vijana 331 wachaguliwa kujiunga na mafunzo idara ya uhamiaji

Na Mwandishi Wetu

IDARA ya Uhamiaji Tanzania imetangaza majina ya vijana 331 waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya idara hiyo kuanzia Machi 1, 2025.

Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo hayo limetolewa leo Alhamisi Februari 6, 2025 na Kamishna Jenerali wa idara hiyo.

“Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anawatangazia vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na Idara ya Uhamiaji kuripoti Chuo cha Uhamiaji cha Raphael Kubaga kilichopo Boma Kichakamiba, Wilaya ya Mkinga – Mkoani Tanga, Jumamosi Machi mosi 2025 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana,” imeeleza taarifa hiyo.

Pia, kwa walioomba na kuchaguliwa kupitia Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, wanatakiwa kuripoti Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Unguja (Tunguu) Jumatatu Februari 24, 2025 saa 2:00 asubuhi.

Katika taarifa hiyo vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo hayo wametakiwa kuripoti wakiwa na vyeti halisi vya elimu na fani mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...

Mradi wa upanuzi Kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Kinyerezi I Extension umekamilika

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, amesema kuwa mradi wa upanuzi...

More like this

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

Mwili wa Jenista Mhagama Kuzikwa Jumanne Mbinga, Ruvuma

Na Mwandishi Wetu MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Peramiho (CCM), Jenista Mhagama unatarajiwa kuzikwa...