Vijana 331 wachaguliwa kujiunga na mafunzo idara ya uhamiaji

Na Mwandishi Wetu

IDARA ya Uhamiaji Tanzania imetangaza majina ya vijana 331 waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya idara hiyo kuanzia Machi 1, 2025.

Tangazo la kuitwa kwenye mafunzo hayo limetolewa leo Alhamisi Februari 6, 2025 na Kamishna Jenerali wa idara hiyo.

“Kamishna Jenerali wa Uhamiaji anawatangazia vijana ambao wamechaguliwa kujiunga na Idara ya Uhamiaji kuripoti Chuo cha Uhamiaji cha Raphael Kubaga kilichopo Boma Kichakamiba, Wilaya ya Mkinga – Mkoani Tanga, Jumamosi Machi mosi 2025 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 8:00 mchana,” imeeleza taarifa hiyo.

Pia, kwa walioomba na kuchaguliwa kupitia Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, wanatakiwa kuripoti Afisi ya Uhamiaji Mkoa wa Kusini Unguja (Tunguu) Jumatatu Februari 24, 2025 saa 2:00 asubuhi.

Katika taarifa hiyo vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo hayo wametakiwa kuripoti wakiwa na vyeti halisi vya elimu na fani mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Rais Ruto awasili nchini

Na Mwandishi Wetu Rais wa Kenya, Dk. William Ruto amewasili nchini leo kwa ziara ya...

Didier Drogba atikisa Bunge la Tanzania

Na Mwandishi Wetu Shangwe​  zimetawala  katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma leo Mei 4, 2026,  ...

Makonda aomba sh.525.32 bilioni, maandalizi AFCON yafikia pazuri

 Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda ameomba sh. 525.32...

Waogeleaji 19 wapaa Argeria, kuiwakilisha Tanzania mchuano ya Afrika

Na Winfrida Mtoi JUMLA ya waogeleaji 19 wamekabidhiwa bendera Mei 2, 2026 kwenda kuiwakilisha Tanzania...

More like this

Rais Ruto awasili nchini

Na Mwandishi Wetu Rais wa Kenya, Dk. William Ruto amewasili nchini leo kwa ziara ya...

Didier Drogba atikisa Bunge la Tanzania

Na Mwandishi Wetu Shangwe​  zimetawala  katika Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma leo Mei 4, 2026,  ...

Makonda aomba sh.525.32 bilioni, maandalizi AFCON yafikia pazuri

 Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda ameomba sh. 525.32...