Bei ya Petroli, dizeli zapanda

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji – EWURA, imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya Petroli nchini ambazo zimeanza kutumika kuanzia leo Februari 05, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) leo Februari 5, 2025, bei ya petroli kwa rejareja katika Jiji la Dar es Salaam imeongezeka kwa asilimia 0.957, dizeli kwa asilimia 2.18 na mafuta ya taa kwa asilimia 1.25.

Hii ikiwa na maana kuwa sasa wanunuzi wa mafuta kwa bei ya rejareja katika Jiji la Dar es Salaam watanunua lita moja kwa Sh. 2,820 kwa petroli, dizeli Sh. 2,703 na mafuta ya taa kwa Sh. 2,710.

Bei hizo ni kutoka Sh. 2,793 kwa bei ya petroli ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa Januari mwaka huu, dizeli Sh. 2,644 na mafuta ya taa kwa Sh. 2,676.

spot_img

Latest articles

SGR yapata ajali, TRC yataja chanzo

Na Mwandishi Wetu Treni ya Mwendokasi (SGR) imeacha njia yake na kupata ajali katika eneo...

Yajayo baada ya uchaguzi mkuu yahitaji hekima kubwa

JUMATANO ijayo, OKTOBA 29, 2025, taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linakwenda kuongeza...

Dkt. Matarajio aagiza vifaa vyote vya uhakiki wa jotoardhi Ziwa Ngozi kufika kwa wakati

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika...

More like this

SGR yapata ajali, TRC yataja chanzo

Na Mwandishi Wetu Treni ya Mwendokasi (SGR) imeacha njia yake na kupata ajali katika eneo...

Yajayo baada ya uchaguzi mkuu yahitaji hekima kubwa

JUMATANO ijayo, OKTOBA 29, 2025, taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linakwenda kuongeza...