Bei ya Petroli, dizeli zapanda

Na Mwandishi Wetu, Dodoma 

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji – EWURA, imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya Petroli nchini ambazo zimeanza kutumika kuanzia leo Februari 05, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) leo Februari 5, 2025, bei ya petroli kwa rejareja katika Jiji la Dar es Salaam imeongezeka kwa asilimia 0.957, dizeli kwa asilimia 2.18 na mafuta ya taa kwa asilimia 1.25.

Hii ikiwa na maana kuwa sasa wanunuzi wa mafuta kwa bei ya rejareja katika Jiji la Dar es Salaam watanunua lita moja kwa Sh. 2,820 kwa petroli, dizeli Sh. 2,703 na mafuta ya taa kwa Sh. 2,710.

Bei hizo ni kutoka Sh. 2,793 kwa bei ya petroli ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa Januari mwaka huu, dizeli Sh. 2,644 na mafuta ya taa kwa Sh. 2,676.

spot_img

Latest articles

Waziri Katambi anatengeneza janga kubwa

MEI mwaka huu picha mjongeo ya mahojiano kati ya Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,...

DIB yawaita wananchi kupata elimu ya amana

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahimiza wananchi kutembelea banda lake katika...

Waziri Mkuu: Kafulila kiongozi kijana mwenye upeo mpana

Amtaja Kama Kiongozi Kijana Mwenye Exposure ya Kimataifa Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu wa Jamhuri...

VETA Kihonda yaja na mashine ya kisasa ya kulimia

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Ufundi stadi (VETA) Kihonda, imebuni mashine...

More like this

Waziri Katambi anatengeneza janga kubwa

MEI mwaka huu picha mjongeo ya mahojiano kati ya Inspekta Jenerali wa Polisi Mstaafu,...

DIB yawaita wananchi kupata elimu ya amana

Na Mwandishi Wetu BODI ya Bima ya Amana (DIB) imewahimiza wananchi kutembelea banda lake katika...

Waziri Mkuu: Kafulila kiongozi kijana mwenye upeo mpana

Amtaja Kama Kiongozi Kijana Mwenye Exposure ya Kimataifa Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu wa Jamhuri...