Waziri Chana azitaka Halmashauri zote nchini kulinda wananchi dhidi ya wanyamapori wakali

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi, Dkt. Pindi Chana amezielekeza Halmashauri zote nchini kuchukua jukumu la kulinda wananchi dhidi ya wanyamapori wakali na waharibifu kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na taasisi zake.

Ameyasema hayo leo Februari 04, 2025 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu swali la Mhandisi Ezra John Chiwelesa aliyetaka kujua Serikali ina mpango gani wa kuondoa adha ya uvamizi wa tembo katika Kijiji cha Nyabugombe Kata ya Nyakahura – Biharamulo.

“Katika bajeti za Halmashauri asilimia 10 za bajeti za Halmashauri, mapato ya ndani na kuna maeneo Wizara ya Maliasili na Utalii inarudisha fedha za Wildlife Management Areas asilimia 25, fedha hizi zinatakiwa zitumike kwa shughuli rafiki za uhifadhi kulinda wananchi wasiumizwe,” amesisitiza Chana.

Amesema kuwa ajenda ya kulinda wananchi dhidi ya changamoto mbalimbali ikiwemo za wanyamapori wakali na waharibifu ni ajenda ya Halmashauri husika na kusisitiza kwamba halmashauri zina uwezo wa kununua ndege nyuki “drones”, kusomesha vijana kozi za uhifadhi ili wawe Askari wa Vijiji wajue namna ya kulinda wananchi.

Awali akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dunstan Kitandula amesema kuwa Serikali inaendelea kutekeleza mikakati mbalimbali ya kukabiliana na adha ya wanyamapori wakali na waharibifu wakiwemo tembo katika maeneo yanayopakana na Hifadhi ya Taifa Burigi – Chato.

“Mikakati inayotekelezwa ni pamoja na: kuendelea kushirikiana na Wananchi kudhibiti tembo kwa wakati ambapo jumla ya Askari sita (6) wa uhifadhi kwa kushirikiana na mgambo sita (6) waliopewa mafunzo kuhusu tabia za wanyamapori wanatumika kufukuza tembo kupitia kituo cha Nyungwe kilichopo Kijiji cha Nyabugombe, Kata ya Nyakahura” amesema Kitandula.

Kijiji cha Nyabugombe kilichopo katika Kata ya Nyakahura, ni miongoni mwa vijiji 38 vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa Burigi-Chato. Kwa kipindi cha miezi sita Julai – Disemba, 2024 Jumla ya matukio 16 ya tembo yaliripotiwa na kudhibitiwa katika kijiji cha Nyabugombe kilichopo Kata ya Nyakahura, Wilaya ya Biharamulo.

spot_img

Latest articles

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

More like this

Mexico yatwaa taji la Miss Universe 2025, Ivory Coast namba tano

Na Mwandishi Wetu Mexico imeibuka mshindi wa taji la Miss Universe 2025 kupitia mrembo wake...

Kocha Yanga ataja mbinu kuingamiza FAR Rabat

Na Mwandishi Wetu KOCHA Mkuu wa Yanga, Pedro Concalves amesema falsafa yake katika mechi ya...

Zawadi za PIKU zafungua milango ya ujasiriamali kwa Watanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA kudhihirisha kuwa teknolojia inabadilisha maisha ya Watanzania, Jukwaa la Kidijitali...