Kapinga: Azma ya serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika wakati wote

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema ni azma ya Serikali kuhakikisha wananchi wanapata umeme wa uhakika na unaotabirika kwa ajili ya shughuli za kijamii na kimaendeleo.

Kapinga ameyasema hayo leo Januari 03, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Lushoto, Shabani Shekilindi aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itaondoa changamoto ya kukatika umeme katika Wilaya ya Lushoto kwa kuweka suluhisho la kudumu.

“Tutafuatilia kwa hii wiki moja kufahamu ni nini changamoto ya kukatika kwa umeme Wilaya ya Lushoto, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge iwapo kuna matengenezo tutahakikisha yanakamilika kwa haraka,” amesisitiza Kapinga.

Akijibu swali Mbunge wa Nkasi Kusini, Vicent Mbogo aliyetaka kufahamu uwepo wa nishati ya umeme katika Kijiji cha Msamba-Masokolo, Lyapinda, Izinga na Lyele na katika Vitongoji vya Kisenga na Lupata, Kapinga amesema Wilaya ya Nkasi ina jumla ya vijiji 90 ambapo vyote vimepatiwa huduma ya umeme vikiwemo vijiji vya Lyele na Lyapinda.

Aidha, amesema Kitongoji cha Lupata kilichopo katika Kijiji cha Lyapinda kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya Mbunge utakaotekelezwa na Mkandarasi aitwae M/s STEG International Services Ltd ambaye ameshakamilisha hatua za upimaji na usanifu.

Ameongeza kuwa, uhakiki wa Kitongoji cha Kisenga umekamilika na Kitongoji hicho kitapatiwa umeme kupitia mradi wa vitongoji (HEP IIB).

spot_img

Latest articles

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Dharura wa SADC kwa njia ya mtandao

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya...

Majaliwa azindua Kituo cha Mabasi Nzega Mjini

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 amezindua kituo kipya...

SEforALL kuimarisha ushirikiano upatikanaji nishati endelevu

📌 Dkt. Biteko asema Nishati Safi ya Kupikia ni ajenda endelevu 📌 Rais...

Umeme wa nje: Tutaepuka vipi vipigo vya nyuma?

Mwanzoni mwa wiki hii iliibuka habari kubwa iliyotokana na tamko la Rais wa Jamhuri...

More like this

Rais Samia ashiriki Mkutano wa Dharura wa SADC kwa njia ya mtandao

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya...

Majaliwa azindua Kituo cha Mabasi Nzega Mjini

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 amezindua kituo kipya...

SEforALL kuimarisha ushirikiano upatikanaji nishati endelevu

📌 Dkt. Biteko asema Nishati Safi ya Kupikia ni ajenda endelevu 📌 Rais...