WAOKOAJI WA KARIAKOO WALA CHAKULA NA RAIS

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi Januari 30, 2025  amekula chakula cha mchana pamoja na   walioshiriki uokoaji katika jengo la ghorofa lililoporomoka Kariakoo Novemba 2024.

Katika hafla hiyo ya chakula cha mchana, Rais Samia amezungumza mambo mbalimbali, huku akimtaka Waziri wa Biashara kuangaliwa suala la wageni kufanya biashara inayofanywa na wenyeji.

“Haiwezekani mgeni akawe mmachinga, vijana wetu watafanya kazi gani, kwa hiyo waziri wa biashara simamia hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha ameeleza kuwa kupitia  mradi wa DMDP, wamejipanga kujenga soko lingine zuri kama lilivyo la Kariakoo katika eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam, hivyo baadhi ya wafanya biashara watahamishwa kwenda kwenye soko hilo.

Kuhusu kuporomoka kwa jengo la Kariakoo, amesema  kumewapa somo na huenda mali zinazofichwa humo hazilipiwi kodi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema Kamati maalumu iliyoundwa kuchunguza kuporomoka kwa jengo la Kariakoo na kufanya ukaguzi wa kina wa majengo yaliyopo katika eneo hilo imekamilisha kazi yake na imewasilisha taarifa itakayokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni

spot_img

Latest articles

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...

CRDB yashirikiana na Kids’ Holiday Festival kukuza elimu ya fedha kwa watoto

Na Mwandishi Wetu BENKI ya CRDB imeingia makubaliano ya ushirikiano na Kids’ Holiday Festival...

More like this

Sekta ya Viwanda na Biashara yazidi kutoa fursa kwa vijana

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga amesema sekta ya viwanda...

Polisi yachunguza tukio la kuchoma moto magari msibani

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro limesema linachunguza tukio la kuchoma moto na...

Taifa Stars yakabidhiwa bendera tayari kwa AFCON 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, ameiaga na...