WAOKOAJI WA KARIAKOO WALA CHAKULA NA RAIS

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi Januari 30, 2025  amekula chakula cha mchana pamoja na   walioshiriki uokoaji katika jengo la ghorofa lililoporomoka Kariakoo Novemba 2024.

Katika hafla hiyo ya chakula cha mchana, Rais Samia amezungumza mambo mbalimbali, huku akimtaka Waziri wa Biashara kuangaliwa suala la wageni kufanya biashara inayofanywa na wenyeji.

“Haiwezekani mgeni akawe mmachinga, vijana wetu watafanya kazi gani, kwa hiyo waziri wa biashara simamia hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha ameeleza kuwa kupitia  mradi wa DMDP, wamejipanga kujenga soko lingine zuri kama lilivyo la Kariakoo katika eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam, hivyo baadhi ya wafanya biashara watahamishwa kwenda kwenye soko hilo.

Kuhusu kuporomoka kwa jengo la Kariakoo, amesema  kumewapa somo na huenda mali zinazofichwa humo hazilipiwi kodi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema Kamati maalumu iliyoundwa kuchunguza kuporomoka kwa jengo la Kariakoo na kufanya ukaguzi wa kina wa majengo yaliyopo katika eneo hilo imekamilisha kazi yake na imewasilisha taarifa itakayokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni

spot_img

Latest articles

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...

Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter...

TCAA yaimarisha usalama wa anga kwa mifumo ya kisasa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), imejizatiti kuendana na mabadiliko...

More like this

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...

Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter...