WAOKOAJI WA KARIAKOO WALA CHAKULA NA RAIS

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi Januari 30, 2025  amekula chakula cha mchana pamoja na   walioshiriki uokoaji katika jengo la ghorofa lililoporomoka Kariakoo Novemba 2024.

Katika hafla hiyo ya chakula cha mchana, Rais Samia amezungumza mambo mbalimbali, huku akimtaka Waziri wa Biashara kuangaliwa suala la wageni kufanya biashara inayofanywa na wenyeji.

“Haiwezekani mgeni akawe mmachinga, vijana wetu watafanya kazi gani, kwa hiyo waziri wa biashara simamia hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha ameeleza kuwa kupitia  mradi wa DMDP, wamejipanga kujenga soko lingine zuri kama lilivyo la Kariakoo katika eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam, hivyo baadhi ya wafanya biashara watahamishwa kwenda kwenye soko hilo.

Kuhusu kuporomoka kwa jengo la Kariakoo, amesema  kumewapa somo na huenda mali zinazofichwa humo hazilipiwi kodi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema Kamati maalumu iliyoundwa kuchunguza kuporomoka kwa jengo la Kariakoo na kufanya ukaguzi wa kina wa majengo yaliyopo katika eneo hilo imekamilisha kazi yake na imewasilisha taarifa itakayokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni

spot_img

Latest articles

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

More like this

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...