WAOKOAJI WA KARIAKOO WALA CHAKULA NA RAIS

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi Januari 30, 2025  amekula chakula cha mchana pamoja na   walioshiriki uokoaji katika jengo la ghorofa lililoporomoka Kariakoo Novemba 2024.

Katika hafla hiyo ya chakula cha mchana, Rais Samia amezungumza mambo mbalimbali, huku akimtaka Waziri wa Biashara kuangaliwa suala la wageni kufanya biashara inayofanywa na wenyeji.

“Haiwezekani mgeni akawe mmachinga, vijana wetu watafanya kazi gani, kwa hiyo waziri wa biashara simamia hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha ameeleza kuwa kupitia  mradi wa DMDP, wamejipanga kujenga soko lingine zuri kama lilivyo la Kariakoo katika eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam, hivyo baadhi ya wafanya biashara watahamishwa kwenda kwenye soko hilo.

Kuhusu kuporomoka kwa jengo la Kariakoo, amesema  kumewapa somo na huenda mali zinazofichwa humo hazilipiwi kodi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema Kamati maalumu iliyoundwa kuchunguza kuporomoka kwa jengo la Kariakoo na kufanya ukaguzi wa kina wa majengo yaliyopo katika eneo hilo imekamilisha kazi yake na imewasilisha taarifa itakayokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni

spot_img

Latest articles

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

More like this

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...