Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi yaanza kazi, yakaribisha wananchi kutoa maoni

Na Winfrida Mtoi

Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi nchini, imesema tayari imeanza kazi rasmi, hivyo kutoa wito kwa wananchi kutoa maoni ya kile wanachohotaji kifanyiwe maboresho katika mfumo wa ulipaji na ukusanyaji kodi.

Akizungumza leo Oktoba, 22 2024 Ikulu jijini Dar es Salaam,  Mwenyekiti wa tume hiyo, Balozi Ombeni Sefue amesema wapo tayari kushirikiana na kumsikiliza kila mdau  iwe mmoja mmoja, kupitia vyama vya kitaalamu, jumuiya za biashara na nyingine ili kupata maoni yatakayowasilishwa kwa Rais Dk. Samia Suluhu.

Balozi Sefue amesema lengo ni kuhakikisha kunakuwa na mfumo bora wa kukusanya mapato na itafanya tathimini hiyo kwa kushirikisha wananchi.

“Mtakumbuka kuwa tarehe 4 Oktoba 2024, Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alizindua rasmi Tume ya Kutathmini na Kushauri kuhusu Maboresho ya Kodi.

“Kama mjuavyo Tume hii imeundwa kufuatia malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi, wafanyabiashara na wawekezaji kuhusu kero mbalimbali zinazotokana na mfumo wa kodi nchini,” ameeleza  Mwenyekiti huyo.

Amefafanua kuwa Tume hiyo imepewa miezi sita lakini machakato wa kutoa maoni utachukua kipindi kisichopungua miezi miwili kuanzia sasa, baada ya hapo watachukua mapendekezo hayo, kuyafanyia tathmini na kuyachanganua kabla ya kuwasilisha kwa Rais.

Ameeleza kuwa wameandaa namna bora ya kuratibu  ushiriki wa wananchi, wafanyabiashara, wawekezaji na taasisi za umma na binafsi, asasi za kiraia, wadau wa maendeleo na wananchi wanaishi nje ya nchi ikiwamo kufanya mikutano katika maeneo mbalimbali.

Balozi Sefue amesema lengo la Serikali imedhamiria  kufikia kiwango  cha asilimia 15 ya pato la Taifa  ifikapo mwaka 2026/27  hatua itakayoongeza  uwezo wa nchi kugharamia miradi ya maendeleo na kupunguza kiwango cha utegemezi wa mikopo na misaada.



spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...