Watu wawili wafariki, 16 wajeruhiwa katika ajali ya basi Songwe

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 16 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga daraja na kutumbukia mtoni katika eneo la Mlima Myovizi, mkoani Songwe.

Ajali hiyo, iliyotokea leo Julai 15 saa 12 asubuhi, ilihusisha basi la Ngasere High Class lililokuwa likisafiri kutoka Dodoma kwenda Tunduma, mkoani Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Gallus Hyera, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo viwili na majeruhi 16 katika ajali hiyo, ambayo ilitokea baada ya basi hilo kugonga nguzo ya daraja na kutumbukia mtoni.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dk. Kelvin Masae, amethibitisha kupokea majeruhi 16 ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wakipewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

spot_img

Latest articles

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

Yanga yatua Zanzibar kuitengenezea dozi AS FAR Rabat

Na Winfrida Mtoi Kikosi cha Yanga kimetua visiwani Zanzibar kwa maandalizi ya kuikabili AS FAR...

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...

More like this

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

Yanga yatua Zanzibar kuitengenezea dozi AS FAR Rabat

Na Winfrida Mtoi Kikosi cha Yanga kimetua visiwani Zanzibar kwa maandalizi ya kuikabili AS FAR...

Rais Samia atangaza Baraza Jipya la Mawaziri, nane watemwa

Tatu Mohamed na Winfrida Mtoi RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan,...