Watu wawili wafariki, 16 wajeruhiwa katika ajali ya basi Songwe

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 16 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga daraja na kutumbukia mtoni katika eneo la Mlima Myovizi, mkoani Songwe.

Ajali hiyo, iliyotokea leo Julai 15 saa 12 asubuhi, ilihusisha basi la Ngasere High Class lililokuwa likisafiri kutoka Dodoma kwenda Tunduma, mkoani Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Gallus Hyera, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo viwili na majeruhi 16 katika ajali hiyo, ambayo ilitokea baada ya basi hilo kugonga nguzo ya daraja na kutumbukia mtoni.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dk. Kelvin Masae, amethibitisha kupokea majeruhi 16 ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wakipewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

spot_img

Latest articles

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko...

Aibu: Ukaburu waibuka Baraza la Wawakilishi

MSIMU wa siasa za masimango na kubaguana umerejea tena na kushika kasi. Safari hii...

BODI YA DAWASA YAINGIA MTAANI KUKAGUA UPATIKANAJI WA MAJI

Na Mwandishi Wetu BODI ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira...

More like this

WANANCHI MSIHOFU KUTUMIA NISHATI YA UMEME KATIKA VYOMBO VYA USAFIRI -MD TWANGE

📌Asema TANESCO inajenga vituo vya kuchajia vyombo hivyo nchi nzima 📌Aeleza mpango wa kusambaza majiko...

Aibu: Ukaburu waibuka Baraza la Wawakilishi

MSIMU wa siasa za masimango na kubaguana umerejea tena na kushika kasi. Safari hii...