Watu wawili wafariki, 16 wajeruhiwa katika ajali ya basi Songwe

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Watu wawili wamefariki dunia na wengine 16 kujeruhiwa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kugonga daraja na kutumbukia mtoni katika eneo la Mlima Myovizi, mkoani Songwe.

Ajali hiyo, iliyotokea leo Julai 15 saa 12 asubuhi, ilihusisha basi la Ngasere High Class lililokuwa likisafiri kutoka Dodoma kwenda Tunduma, mkoani Songwe.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, Gallus Hyera, amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo viwili na majeruhi 16 katika ajali hiyo, ambayo ilitokea baada ya basi hilo kugonga nguzo ya daraja na kutumbukia mtoni.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mbozi, Dk. Kelvin Masae, amethibitisha kupokea majeruhi 16 ambao wanaendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wakipewa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe.

spot_img

Latest articles

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

Tanzania kujifunza kutoka China kuhusu mageuzi ya mashirika ya umma

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam TANZANIA imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China...

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yafanya mazungumzo na Balozi wa China

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam OFISI ya Msajili wa Hazina imekutana na kufanya...

More like this

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

Tanzania kujifunza kutoka China kuhusu mageuzi ya mashirika ya umma

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam TANZANIA imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China...

Naibu Waziri Nishati aitaka Tanesco kuimarisha huduma kwa wateja kupitia mifumo ya kidigitali

📌 Afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka 2026 wa Maafisa Uhusiano na Huduma kwa Wateja...