UVCCM yaukataa mtandao wa X

Na Winfrida Mtoi

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umeishauri Serikali kuchunguza maudhui yaliyomo katika Mtandao wa X (zamani Twitter) kwa kile wanachodai kuwa yanakwenda kinyume na mila na desturi za Watanzania.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UVCCM, Mohammed Kawaida wakati akizungumza na waandishi wa habari Juni 11,2024, jijini Dar es Salaam.

Amesema baadhi ya maudhui yanayotolewa katika mtandao huo yanaweza kusababisha mmomonyoko wa maadili nchini.

“Maudhui ya kingono na mengine si utamaduni wa Mtanzania, umefika wakati sasa kwa Serikali kuufungia mtandao huu kwa sababu hauendani na tamaduni zetu.

“Walianza kwa kutuandaa kisaikolojia wamebadilisha jina kutoka Twitter hadi X ili tuone ni neno la kawaida, watu wengi wanatumia mtandao huu hasa vijana Serikali ichukue hatua kulinda maadili ya vijana na Watanzania wote kwa ujumla,” amesema Kawaida.

Julai 2023 Mmiliki wa mtandao huo, Elon Musk, alitangaza mabadiliko ya nembo yake kutoka ndege hadi herufi X.

spot_img

Latest articles

Rais Samia atoa salamu za Rambirambi kwa kifo cha Kardinali Pengo

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma...

Kardinali Polycarp Pengo Afariki Dunia

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,...

TIRDO yapongezwa, yaagizwa kujitangaza zaidi

Na Tatu Mohamed KATIBU Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,...

CRDB, HESLB na Basil Link Wazindua ‘Imbeju – SmartElite’ Kuinua Vijana Kidijitali

Na Mwandishi Wetu Benki ya CRDB Bank kupitia CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na...

More like this

Rais Samia atoa salamu za Rambirambi kwa kifo cha Kardinali Pengo

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametuma...

Kardinali Polycarp Pengo Afariki Dunia

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam,...

TIRDO yapongezwa, yaagizwa kujitangaza zaidi

Na Tatu Mohamed KATIBU Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Balozi Waziri Salum,...