UVCCM yaukataa mtandao wa X

Na Winfrida Mtoi

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umeishauri Serikali kuchunguza maudhui yaliyomo katika Mtandao wa X (zamani Twitter) kwa kile wanachodai kuwa yanakwenda kinyume na mila na desturi za Watanzania.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UVCCM, Mohammed Kawaida wakati akizungumza na waandishi wa habari Juni 11,2024, jijini Dar es Salaam.

Amesema baadhi ya maudhui yanayotolewa katika mtandao huo yanaweza kusababisha mmomonyoko wa maadili nchini.

“Maudhui ya kingono na mengine si utamaduni wa Mtanzania, umefika wakati sasa kwa Serikali kuufungia mtandao huu kwa sababu hauendani na tamaduni zetu.

“Walianza kwa kutuandaa kisaikolojia wamebadilisha jina kutoka Twitter hadi X ili tuone ni neno la kawaida, watu wengi wanatumia mtandao huu hasa vijana Serikali ichukue hatua kulinda maadili ya vijana na Watanzania wote kwa ujumla,” amesema Kawaida.

Julai 2023 Mmiliki wa mtandao huo, Elon Musk, alitangaza mabadiliko ya nembo yake kutoka ndege hadi herufi X.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...