UVCCM yaukataa mtandao wa X

Na Winfrida Mtoi

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umeishauri Serikali kuchunguza maudhui yaliyomo katika Mtandao wa X (zamani Twitter) kwa kile wanachodai kuwa yanakwenda kinyume na mila na desturi za Watanzania.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa UVCCM, Mohammed Kawaida wakati akizungumza na waandishi wa habari Juni 11,2024, jijini Dar es Salaam.

Amesema baadhi ya maudhui yanayotolewa katika mtandao huo yanaweza kusababisha mmomonyoko wa maadili nchini.

“Maudhui ya kingono na mengine si utamaduni wa Mtanzania, umefika wakati sasa kwa Serikali kuufungia mtandao huu kwa sababu hauendani na tamaduni zetu.

“Walianza kwa kutuandaa kisaikolojia wamebadilisha jina kutoka Twitter hadi X ili tuone ni neno la kawaida, watu wengi wanatumia mtandao huu hasa vijana Serikali ichukue hatua kulinda maadili ya vijana na Watanzania wote kwa ujumla,” amesema Kawaida.

Julai 2023 Mmiliki wa mtandao huo, Elon Musk, alitangaza mabadiliko ya nembo yake kutoka ndege hadi herufi X.

spot_img

Latest articles

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...

Jeshi la Polisi lachunguza  taarifa ya OCD  Chunya

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi limesema limeona na linafanyia uchunguzi taarifa inayosambaa kwenye mitandao...

More like this

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

Ndejembi: Tanzania sasa ina umeme wa kutosha

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amesema Tanzania kwa sasa ina umeme...