Juma Dunia Haji ajitoa kuwania uenyekiti ACT

Mgombea nafasi ya uenyekiti chama cha ACT Wazalendo, Juma Duni Haji (babu Duni) ameamua kujiondoa kwenye kinyanganyiro hicho, ikiwa ni siku moja kabla ya uchaguzi wa mwenyekiti wa chama hicho cha upinzani nchini.Babu Duni amejiondoa katika kinyang’anyiro hicho leo Jumatatu, Mach 4, 2024 wakati akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya ACT – Wazalendo katika ukumbi wa Hakainde Hichilema uliopo makao makuu ya chama hicho, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Duni ambaye alikuwa akigombea kuteteta nafasi yake, amesema ameamua kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumuunga mkono aliyekuwa mshindani wake pekee, Othman Masoud Othman. Hivyo Othman amebaki kuwa mgombea pekee.

Uamuzi huo wa Babu Duni umekuja saa chache bada ya kuwapo malalamiko yake juu ya kuwapo hujuma za watu waliokuwa wanamshinikiza kujitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa madai kwamba ni mzee, huku kukiwa na taarifa za wenyeviti kadhaa wa mikoa kumchukulia fomu mshindani wake.Hata hivyo, leo, Babu Duni amesema amelazimika kujiondoa baada ya kutafakari kwa kina akijua kuwa chama hicho kina malengo makubwa ya kushika dola, hivyo kubaki kwake bila shaka kungekiletea madhara.

“Nimeamua kujiondoa kuweka heshima kwenye chama kwa sababu tuna muda mfupi kuelelea kwenye uchaguzi, hatuhitaji msuguano,” alisema 

Babu Duni, huku akiwataka viongozi wakuu wa chama hicho watakaochaguliwa kutowatenga kabisa wale wote ambao walikuwa wakimuunga mkono kwenye kampeni zake.Katika hatua nyingine, mgombea nafasi makamu mwenyekiti Zanzibar, Hijja Hassan Hija naye amejiondoa kwenye uchaguzi huo kKpitia barua yake iliyosomwa na Katibu Mkuu, Ado Shaibu, akisema haoni sababu ya kuendelea kugombea, hivyo kumwachia Ismail Jussa Ladhu awe mgombea pekee.

spot_img

Latest articles

Rejoinder: Tanga Is Still the Strategic Bet, and Tanzania Can Win It

By Peter C. Mhando, PhD Amani Mrope is right: capital has memory. But memory cuts...

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

More like this

Rejoinder: Tanga Is Still the Strategic Bet, and Tanzania Can Win It

By Peter C. Mhando, PhD Amani Mrope is right: capital has memory. But memory cuts...

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...