Juma Dunia Haji ajitoa kuwania uenyekiti ACT

Mgombea nafasi ya uenyekiti chama cha ACT Wazalendo, Juma Duni Haji (babu Duni) ameamua kujiondoa kwenye kinyanganyiro hicho, ikiwa ni siku moja kabla ya uchaguzi wa mwenyekiti wa chama hicho cha upinzani nchini.Babu Duni amejiondoa katika kinyang’anyiro hicho leo Jumatatu, Mach 4, 2024 wakati akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu Taifa ya ACT – Wazalendo katika ukumbi wa Hakainde Hichilema uliopo makao makuu ya chama hicho, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Duni ambaye alikuwa akigombea kuteteta nafasi yake, amesema ameamua kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho na kumuunga mkono aliyekuwa mshindani wake pekee, Othman Masoud Othman. Hivyo Othman amebaki kuwa mgombea pekee.

Uamuzi huo wa Babu Duni umekuja saa chache bada ya kuwapo malalamiko yake juu ya kuwapo hujuma za watu waliokuwa wanamshinikiza kujitoa katika kinyang’anyiro hicho kwa madai kwamba ni mzee, huku kukiwa na taarifa za wenyeviti kadhaa wa mikoa kumchukulia fomu mshindani wake.Hata hivyo, leo, Babu Duni amesema amelazimika kujiondoa baada ya kutafakari kwa kina akijua kuwa chama hicho kina malengo makubwa ya kushika dola, hivyo kubaki kwake bila shaka kungekiletea madhara.

“Nimeamua kujiondoa kuweka heshima kwenye chama kwa sababu tuna muda mfupi kuelelea kwenye uchaguzi, hatuhitaji msuguano,” alisema 

Babu Duni, huku akiwataka viongozi wakuu wa chama hicho watakaochaguliwa kutowatenga kabisa wale wote ambao walikuwa wakimuunga mkono kwenye kampeni zake.Katika hatua nyingine, mgombea nafasi makamu mwenyekiti Zanzibar, Hijja Hassan Hija naye amejiondoa kwenye uchaguzi huo kKpitia barua yake iliyosomwa na Katibu Mkuu, Ado Shaibu, akisema haoni sababu ya kuendelea kugombea, hivyo kumwachia Ismail Jussa Ladhu awe mgombea pekee.

spot_img

Latest articles

Yajayo baada ya uchaguzi mkuu yahitaji hekima kubwa

JUMATANO ijayo, OKTOBA 29, 2025, taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linakwenda kuongeza...

Dkt. Matarajio aagiza vifaa vyote vya uhakiki wa jotoardhi Ziwa Ngozi kufika kwa wakati

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika...

Viongozi wa dini Kaskazini wahimiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Moshi VIONGOZI wa dini kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini, wamewataka Watanzania...

Zulfa Macho atinga fainali ya ngumi Zone 3 Afrika

Na Mwandishi Wetu Bondia Mtanzania Zulfa Macho amemchapa kwa pointi Bisambu Deborah wa DR Congo...

More like this

Yajayo baada ya uchaguzi mkuu yahitaji hekima kubwa

JUMATANO ijayo, OKTOBA 29, 2025, taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linakwenda kuongeza...

Dkt. Matarajio aagiza vifaa vyote vya uhakiki wa jotoardhi Ziwa Ngozi kufika kwa wakati

Na Mwandishi Wetu NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameliagiza Shirika...

Viongozi wa dini Kaskazini wahimiza amani kuelekea Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Moshi VIONGOZI wa dini kutoka mikoa ya kanda ya kaskazini, wamewataka Watanzania...