Polisi wawasaka walioua, kukata nyeti za marehemu

Polisi mkoani Mwanza wanawasaka wahusika wa mauaji ya Masanja Kefa (32) mkazi wa Kijiji cha Mwagig’hi, Kata ya Nkalalo wilayani kwimba, kukata sehemu zake za siri kisha kutoweka nazo. Tukio hilo linalohusishwa na imani za ushirikina, Februari 12, 2024.

Ofisa Polisi Jamii Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Sarige amesema wakati polisi wakiedelea na uchunguzi wa tukio hilo, wakazi wa Kijiji cha Mwagig’hi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa ambazo zitawezesha waliotenda uhalifu huo kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

ACP Sarige amesema hayo Februari 26, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wakati wakitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wakazi wa kijiji hicho.

“Tumewaletea Polisi Kata lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi shirikishi lakini mmempokea kwa tukio hili la kikatili, si vyema kuendekeza vitendo hivi vya kishirikiana, tuhakikishe tunashirikiana katika ulinzi shirikishi ili kukomesha vitendo hivi,”anasema Sarige na kuongeza:

“Tunajua watu hawa mnawafahamu na wengine wanaweza kuwa ni ndugu zetu, hivyo tusiwafiche wahalifu hawa kwani leo kwake, kesho kwako. Kama kafanya hivyo kwa huyo, umemtunza kesho atakufanyia wewe.”

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamewapongeza polisi kwa kuimarisha ushirikiano na kuwa karibu hasa wakati huu ambao wamesema ni mgumu, na wameahidi kutoa ushirikiano ili kuwapata wahalifu waliohusika na tukio.

spot_img

Latest articles

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

More like this

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...