Polisi wawasaka walioua, kukata nyeti za marehemu

Polisi mkoani Mwanza wanawasaka wahusika wa mauaji ya Masanja Kefa (32) mkazi wa Kijiji cha Mwagig’hi, Kata ya Nkalalo wilayani kwimba, kukata sehemu zake za siri kisha kutoweka nazo. Tukio hilo linalohusishwa na imani za ushirikina, Februari 12, 2024.

Ofisa Polisi Jamii Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ramadhani Sarige amesema wakati polisi wakiedelea na uchunguzi wa tukio hilo, wakazi wa Kijiji cha Mwagig’hi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa ambazo zitawezesha waliotenda uhalifu huo kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

ACP Sarige amesema hayo Februari 26, 2024 akiwa ameambatana na baadhi ya maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wakati wakitoa elimu ya Polisi Jamii kwa wakazi wa kijiji hicho.

“Tumewaletea Polisi Kata lengo likiwa ni kuimarisha ulinzi shirikishi lakini mmempokea kwa tukio hili la kikatili, si vyema kuendekeza vitendo hivi vya kishirikiana, tuhakikishe tunashirikiana katika ulinzi shirikishi ili kukomesha vitendo hivi,”anasema Sarige na kuongeza:

“Tunajua watu hawa mnawafahamu na wengine wanaweza kuwa ni ndugu zetu, hivyo tusiwafiche wahalifu hawa kwani leo kwake, kesho kwako. Kama kafanya hivyo kwa huyo, umemtunza kesho atakufanyia wewe.”

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wamewapongeza polisi kwa kuimarisha ushirikiano na kuwa karibu hasa wakati huu ambao wamesema ni mgumu, na wameahidi kutoa ushirikiano ili kuwapata wahalifu waliohusika na tukio.

spot_img

Latest articles

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...

Watumishi wa umma waaswa kushiriki Uchaguzi wa Oktoba 29

Dar es Salaam. Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH) imetoa wito kwa watumishi wote...

More like this

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

Viongozi wa dini waendelea kihimiza amani uchaguzi mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam VIONGOZI wa dini nchini wameendelea kuhimiza umuhimu wa kudumisha...

Ujumbe wa viongozi wa dini kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025 katika Kongamano la Kamati ya Amani Kitaifa Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu Askofu Mkuu Wapo Mission, Dk. Sylvester Gamanywa “Mungu ambaye tunamwakilisha ndiye anayweka watawala...