Chadema yaongoza maandamano Arusha

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaongoza Maandamano ya amani jijini Arusha, likiwa ni hitimisho la awamu ya kwanza ya maandamano yaliyoogozwa na chama hicho katika mikoa minne nchni.

Tayari chama hicho kimefanya maandamano kama hayo katika makao makuu ya mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya. Maandamano hayo yanaonozwa na viongozi wakuu wa chama hicho, wakiwamo Mwenyekiti Freeman Mbowe, Maksmu Mwenyekiti (Bara), Tundu Lissu na Katibu Mkuu, John Mnyika. Kwa mujibu wa Msimamizi wa maandamano ya Kanda ya Kaskazini, Salum Mwalimu maandamano hayo nayatarajiwa kuhitimishwa alasiri kwa mkutano wa hadhara uliopangwa kufanyika uwanja wa reli.

Lengo la maandamano hayo yaliyopewa jina la ‘vuguvugu la haki ya Watanzania’ ni kuishinikiza Serikali kushughulikia tatizo la gharama za maisha. Pia, kuitaka Serikali kusikiliza maoni ya wananchi kwenye miswada ya uchaguzi iliyokuwa imepelekwa bungeni Novemba 10 mwaka jana na kujadiliwa katika mkutano wa bungeni kisha kupitishwa na sasa inasubiriwa kusainiwa na Rais kuwa sheria.



Maandamano hayo yalianzia jijini Dar es Salaam kwenda Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN), zilizopo Ubungo, kufikisha ujumbe wao huo, wakati yale ya jijini Mwanza yalimalizika kwa mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Furahisha na jijini Mbeya yalihitimisha pia kwa mkutano kama huo Viwanja vya Rwanda Nzovwe.

spot_img

Latest articles

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...

Ofisi ya Msajili wa Hazina yalenga kukusanya Sh2 trilioni mwaka 2026/27

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) imejiwekea lengo la kukusanya Sh2...

More like this

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Sangweni: Sekta ya Mafuta na Gesi Ni Chachu ya Ukuaji wa Uchumi wa Taifa

Na Mwandishi Wetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli...

VETA Kihonda yaja ‘cold room’ kupunguza upotevu wa mazao ya wakulima

Na Mwandishi Wetu UBUNIFU wa mfumo jumuishi wa kuhifadhi mazao kwa kutumia teknolojia ya ubaridi...