Chadema yaongoza maandamano Arusha

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaongoza Maandamano ya amani jijini Arusha, likiwa ni hitimisho la awamu ya kwanza ya maandamano yaliyoogozwa na chama hicho katika mikoa minne nchni.

Tayari chama hicho kimefanya maandamano kama hayo katika makao makuu ya mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya. Maandamano hayo yanaonozwa na viongozi wakuu wa chama hicho, wakiwamo Mwenyekiti Freeman Mbowe, Maksmu Mwenyekiti (Bara), Tundu Lissu na Katibu Mkuu, John Mnyika. Kwa mujibu wa Msimamizi wa maandamano ya Kanda ya Kaskazini, Salum Mwalimu maandamano hayo nayatarajiwa kuhitimishwa alasiri kwa mkutano wa hadhara uliopangwa kufanyika uwanja wa reli.

Lengo la maandamano hayo yaliyopewa jina la ‘vuguvugu la haki ya Watanzania’ ni kuishinikiza Serikali kushughulikia tatizo la gharama za maisha. Pia, kuitaka Serikali kusikiliza maoni ya wananchi kwenye miswada ya uchaguzi iliyokuwa imepelekwa bungeni Novemba 10 mwaka jana na kujadiliwa katika mkutano wa bungeni kisha kupitishwa na sasa inasubiriwa kusainiwa na Rais kuwa sheria.



Maandamano hayo yalianzia jijini Dar es Salaam kwenda Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN), zilizopo Ubungo, kufikisha ujumbe wao huo, wakati yale ya jijini Mwanza yalimalizika kwa mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Furahisha na jijini Mbeya yalihitimisha pia kwa mkutano kama huo Viwanja vya Rwanda Nzovwe.

spot_img

Latest articles

Mlugu Mtanzania wa kwanza kutinga robo fainali mashindano ya Judo Jumuiya ya Madola 2026

Glasgow, Scotland Mchezaji wa Judu, Andrew Mlugu, ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kutinga...

FURSA ZA BIASHARA ZA MABILIONI KATIKA MIGODI ZAWAFUNGUKIA WATANZANIA

Vijana na wanawake wapewa kipaumbele kunufaika na mnyororo wa thamani wa madini Na Mwandishi Wetu...

GST yaongeza kasi ya tafiti za kijiosayansi kuvutia uwekezaji sekta ya madini

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeongeza kasi ya...

UDSM wabuni mfumo wa simu janja unaosaidia wakulima kutumia maji kwa ufanisi

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaotumia...

More like this

Mlugu Mtanzania wa kwanza kutinga robo fainali mashindano ya Judo Jumuiya ya Madola 2026

Glasgow, Scotland Mchezaji wa Judu, Andrew Mlugu, ameweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kutinga...

FURSA ZA BIASHARA ZA MABILIONI KATIKA MIGODI ZAWAFUNGUKIA WATANZANIA

Vijana na wanawake wapewa kipaumbele kunufaika na mnyororo wa thamani wa madini Na Mwandishi Wetu...

GST yaongeza kasi ya tafiti za kijiosayansi kuvutia uwekezaji sekta ya madini

Na Mwandishi Wetu TAASISI ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) imeongeza kasi ya...