Chadema yaongoza maandamano Arusha

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaongoza Maandamano ya amani jijini Arusha, likiwa ni hitimisho la awamu ya kwanza ya maandamano yaliyoogozwa na chama hicho katika mikoa minne nchni.

Tayari chama hicho kimefanya maandamano kama hayo katika makao makuu ya mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya. Maandamano hayo yanaonozwa na viongozi wakuu wa chama hicho, wakiwamo Mwenyekiti Freeman Mbowe, Maksmu Mwenyekiti (Bara), Tundu Lissu na Katibu Mkuu, John Mnyika. Kwa mujibu wa Msimamizi wa maandamano ya Kanda ya Kaskazini, Salum Mwalimu maandamano hayo nayatarajiwa kuhitimishwa alasiri kwa mkutano wa hadhara uliopangwa kufanyika uwanja wa reli.

Lengo la maandamano hayo yaliyopewa jina la ‘vuguvugu la haki ya Watanzania’ ni kuishinikiza Serikali kushughulikia tatizo la gharama za maisha. Pia, kuitaka Serikali kusikiliza maoni ya wananchi kwenye miswada ya uchaguzi iliyokuwa imepelekwa bungeni Novemba 10 mwaka jana na kujadiliwa katika mkutano wa bungeni kisha kupitishwa na sasa inasubiriwa kusainiwa na Rais kuwa sheria.



Maandamano hayo yalianzia jijini Dar es Salaam kwenda Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN), zilizopo Ubungo, kufikisha ujumbe wao huo, wakati yale ya jijini Mwanza yalimalizika kwa mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Furahisha na jijini Mbeya yalihitimisha pia kwa mkutano kama huo Viwanja vya Rwanda Nzovwe.

spot_img

Latest articles

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 220 IGANJO–SAZA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA UCHIMBAJI WA MADINI – MHE. SALOME

📌 Ashuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza,...

Salome Ashuhudia utiaji saini mkataba wa sh. bilioni 198 kuimarisha umeme Songwe, Chunya

📌Ataka kasi ya utekelezaji wa mradi na wazawa kupewa kipaumbele 📌Wachimbaji wapongeza Na Mwandishi Wetu NAIBU...

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

More like this

TANZANIA YAZIDI KUIMARISHA NAFASI YAKE KATIKA BIASHARA YA UMEME KIKANDA

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar TANZANIA imeendelea kuimarisha nafasi yake katika biashara ya umeme kikanda, huku...

MRADI WA NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME WA KV 220 IGANJO–SAZA KUIMARISHA UPATIKANAJI WA UMEME NA KUCHOCHEA UCHIMBAJI WA MADINI – MHE. SALOME

📌 Ashuhudia utiaji saini mkataba wa utekelezaji wa mradi kutoka Iganjo, Mbeya hadi Saza,...

Salome Ashuhudia utiaji saini mkataba wa sh. bilioni 198 kuimarisha umeme Songwe, Chunya

📌Ataka kasi ya utekelezaji wa mradi na wazawa kupewa kipaumbele 📌Wachimbaji wapongeza Na Mwandishi Wetu NAIBU...