Chadema yaongoza maandamano Arusha

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaongoza Maandamano ya amani jijini Arusha, likiwa ni hitimisho la awamu ya kwanza ya maandamano yaliyoogozwa na chama hicho katika mikoa minne nchni.

Tayari chama hicho kimefanya maandamano kama hayo katika makao makuu ya mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Mbeya. Maandamano hayo yanaonozwa na viongozi wakuu wa chama hicho, wakiwamo Mwenyekiti Freeman Mbowe, Maksmu Mwenyekiti (Bara), Tundu Lissu na Katibu Mkuu, John Mnyika. Kwa mujibu wa Msimamizi wa maandamano ya Kanda ya Kaskazini, Salum Mwalimu maandamano hayo nayatarajiwa kuhitimishwa alasiri kwa mkutano wa hadhara uliopangwa kufanyika uwanja wa reli.

Lengo la maandamano hayo yaliyopewa jina la ‘vuguvugu la haki ya Watanzania’ ni kuishinikiza Serikali kushughulikia tatizo la gharama za maisha. Pia, kuitaka Serikali kusikiliza maoni ya wananchi kwenye miswada ya uchaguzi iliyokuwa imepelekwa bungeni Novemba 10 mwaka jana na kujadiliwa katika mkutano wa bungeni kisha kupitishwa na sasa inasubiriwa kusainiwa na Rais kuwa sheria.



Maandamano hayo yalianzia jijini Dar es Salaam kwenda Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN), zilizopo Ubungo, kufikisha ujumbe wao huo, wakati yale ya jijini Mwanza yalimalizika kwa mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Furahisha na jijini Mbeya yalihitimisha pia kwa mkutano kama huo Viwanja vya Rwanda Nzovwe.

spot_img

Latest articles

Waziri Ndejembi afungua kikao cha 55 cha Baraza Kuu la wafanyakazi wa Tanesco Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, leo tarehe 22 Januari, 2026 amefungua...

Waziri Mkuu ataka kazi za Serikali zifanyike Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inataka kazi zote zifanyike makao...

Mzee Mtei kuzikwa Jumamosi Tengeru

Na Mwandishi Wetu MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mzee Edwin Mtei anatarajiwa...

More like this

Waziri Ndejembi afungua kikao cha 55 cha Baraza Kuu la wafanyakazi wa Tanesco Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, leo tarehe 22 Januari, 2026 amefungua...

Waziri Mkuu ataka kazi za Serikali zifanyike Dodoma

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali inataka kazi zote zifanyike makao...