Waliotafuna fedha za AMCOS Mbozi waanza ‘kuzitapika

SHILINGI milioni 170 ambazo ni sehemu ya mamilioni ya fedha zilizobainika kutafunwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika (AMCOS) vinane katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, zimerejeshwa.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema leo bungeni Dodoma kuwa fedha hizo ni sehemu ya Sh. Milioni 294 ambazo serikali inaendelea kupambana ili kuzirejesha kwa wakulima.

Akijibu swali la mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole, Bashe amesema mpaka sasa vyama vya ushirika 20 vimechunguzwa na vinane (8) vimebainika kufanya ubadhirifu na wahusika wamechukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Mbunge Mwenisongole alitaka kufahamu lini serikali itaanza uchunguzi kwa vyama vya (AMCOS) ambavyo awali havikufanyiwa uchunguzi dhidi ya tuhuma za ubadhirifu kwa wakulima.

Bashe amesema unaofanywa kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika utazifikia AMCOS 98 za wilayani Mbozi na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2024.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...