Waliotafuna fedha za AMCOS Mbozi waanza ‘kuzitapika

SHILINGI milioni 170 ambazo ni sehemu ya mamilioni ya fedha zilizobainika kutafunwa baadhi ya viongozi wa vyama vya ushirika (AMCOS) vinane katika wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, zimerejeshwa.

Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema leo bungeni Dodoma kuwa fedha hizo ni sehemu ya Sh. Milioni 294 ambazo serikali inaendelea kupambana ili kuzirejesha kwa wakulima.

Akijibu swali la mbunge wa Mbozi, George Mwenisongole, Bashe amesema mpaka sasa vyama vya ushirika 20 vimechunguzwa na vinane (8) vimebainika kufanya ubadhirifu na wahusika wamechukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Mbunge Mwenisongole alitaka kufahamu lini serikali itaanza uchunguzi kwa vyama vya (AMCOS) ambavyo awali havikufanyiwa uchunguzi dhidi ya tuhuma za ubadhirifu kwa wakulima.

Bashe amesema unaofanywa kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika utazifikia AMCOS 98 za wilayani Mbozi na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2024.

spot_img

Latest articles

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

More like this

Waziri Mkuu atoa sababu yakutotaja idadi vifo vilivyotokea Oktoba 29

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema ni muhimu watanzania kutanguliza utu na...

Niffer arudishwa gerezani, 20 kesi ya uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Watuhumiwa 20 kati ya 22 waliokuwa wanashtakiwa kwa makosa ya uhaini wameachiwa...

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...