102 wafutiwa matokeo ya kidato cha nne

Na Esther Mnyika

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA),  limefuta matokeo  ya watahiniwa 102 wa mtihani wa kidato cha nne mwaka 2023 kutokana na udanganyifu na   waliondika lugha ya matusi kwenye karatasi za majibu.

Matokeo ya  ya kitado cha nne yametangazwa  leo Januari 25, 2024 jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa  NECTA, Dk.Said Mohamed.

Amesema  kati  hao waliofutiwa matokeo, watano  waliondika matusi, wakati  matokeo ya wanafunzi 376 yakizuiwa kutokana na kupata  matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani.

Dk.Mohamed amesema watahiniwa walioshindwa kufanya mtihani huo mwaka jana  wamepewa fursa ya kufanya masomo ambayo hawakuyafanya kwa sababu ya ugonjwa  kwa mujibu wa Kifungu cha 32(1) cha Kanuni za Mitihani.

Dk. Mohammed amesema jumla ya watahiniwa 572,359 walisajiliwa kufanya mtihani huo Novemba mwaka jana ambapo 484,823 sawa na asilimia 87.65wamefaulu.

Amesema wasichana waliofaulu ni 257,892,   wavulana wakiwa 226,931, huku masomo ya lugha ikiwamo kichina yakifanya vizuri zaidi.

Amesema  wanafunzi waliofaulu masomo ya kiswahili  asilimia 96.80 na kichina ni 91.36

“Kati ya watahiniwa 471,427 waliofaulu, wasichana ni 250,147 sawa na asilimia 88.11 na wavulana ni 221,280 sawa na asilimia 90.81. Hivyo, wavulana wamefaulu vizuri zaidi kuliko wasichana,” amesema.

Hata hivyo NECTA imezipongeza  Kamati za Uendeshaji Mitihani za Mikoa na Halmashauri, Manispaa na Jiji, wakuu wa shule, wasimamizi na wasahihishaji wa mtihani huo  kwa kazi nzuri ya kutekeleza jukumu la uendeshaji  mtihani huo.










spot_img

Latest articles

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...

MHANDISI SWEDI: NANENANE NI FURSA YA KUIMARISHA SEKTA YA MADINI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, amesema...

Zimamoto yatoa elimu ya uokoaji, yakazia hatua za awali wakati wa majanga

Na Mwandishi Wetu, Dodoma JESHI la Zimamoto na Uokoaji limeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu...

More like this

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...

MHANDISI SWEDI: NANENANE NI FURSA YA KUIMARISHA SEKTA YA MADINI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, amesema...