102 wafutiwa matokeo ya kidato cha nne

Na Esther Mnyika

Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA),  limefuta matokeo  ya watahiniwa 102 wa mtihani wa kidato cha nne mwaka 2023 kutokana na udanganyifu na   waliondika lugha ya matusi kwenye karatasi za majibu.

Matokeo ya  ya kitado cha nne yametangazwa  leo Januari 25, 2024 jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa  NECTA, Dk.Said Mohamed.

Amesema  kati  hao waliofutiwa matokeo, watano  waliondika matusi, wakati  matokeo ya wanafunzi 376 yakizuiwa kutokana na kupata  matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani.

Dk.Mohamed amesema watahiniwa walioshindwa kufanya mtihani huo mwaka jana  wamepewa fursa ya kufanya masomo ambayo hawakuyafanya kwa sababu ya ugonjwa  kwa mujibu wa Kifungu cha 32(1) cha Kanuni za Mitihani.

Dk. Mohammed amesema jumla ya watahiniwa 572,359 walisajiliwa kufanya mtihani huo Novemba mwaka jana ambapo 484,823 sawa na asilimia 87.65wamefaulu.

Amesema wasichana waliofaulu ni 257,892,   wavulana wakiwa 226,931, huku masomo ya lugha ikiwamo kichina yakifanya vizuri zaidi.

Amesema  wanafunzi waliofaulu masomo ya kiswahili  asilimia 96.80 na kichina ni 91.36

“Kati ya watahiniwa 471,427 waliofaulu, wasichana ni 250,147 sawa na asilimia 88.11 na wavulana ni 221,280 sawa na asilimia 90.81. Hivyo, wavulana wamefaulu vizuri zaidi kuliko wasichana,” amesema.

Hata hivyo NECTA imezipongeza  Kamati za Uendeshaji Mitihani za Mikoa na Halmashauri, Manispaa na Jiji, wakuu wa shule, wasimamizi na wasahihishaji wa mtihani huo  kwa kazi nzuri ya kutekeleza jukumu la uendeshaji  mtihani huo.










spot_img

Latest articles

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

SAPP kufungua Fursa kwa Tanzania Kuwa Kitovu cha Biashara ya Umeme Kusini mwa Afrika

📌Nchi 18 Zakutana Zanzibar kujadili usalama wa nishati ya umeme kusini mwa Afrika 📌Kuuza au...

More like this

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...