Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Wawekezaji wakumbushwa kuendelea kuchangia katika miradi ya maendeleo

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu), Jenista Mhagam, ametoa rai kwa wawekezaji wa mbalimbali katika jimbo la Peramiho kuendelea Kufanya uwekezaji wenye tija kwa wananchi, kwa Halmashauri na kwa Taifa.

Waziri Mhagama ametoa rai hiyo wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Muhukuru katika ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Songea Julai 12, 2023.

“Tunataka wawekezaji wajue wana wajibu wa kuchangia shughuli za maendeleo kwenye vijiji vinavozunguka maeneo uwekezaji,” amesisitiza.

Makaa ya mawe yamekuwa bidhaa muhimu na adhimu, uwekezaji umeendelea kukua na masoko yameongezeka, wawekezaji waangalie ajira zile zinazosaidia kuendesha miradi yao ili kutoa kipaombele katika maeneo ya vijjiji vilivyozunguka mradi, alisema Waziri Mhagama.

“Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi nzuri ya kuvutia Wawekezaji Mbalimbali, Wawekezaji wa shamba la miwa, wawekezaji wa makaa ya mawe na wawekezaji wa umeme wa maji, naomba kila Mwekezaji aliyeomba ardhi ya uwekezaji atumie kama alivyoomba,” amesema Mhagama.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea, Menas Komba amesema uwekezaji wa makaa ya mawe kuna mpango kabambe ambao umelenga kupata asilimia moja ya kila awamu ya mauzo.

“Tuendele kushirikiana na wawekezaji wanaokuja kuwekeza ili waendelee kutusaidia na Halmashauri itasimamia kupata haki za wananchi,” amesema Komba

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Songea, Mwalimu Neema Maghembe amesema wawekezaji wote waliowekeza katika Halmashauri ya Songea wamefuata taratibu zote za uwekezaji.

“Tunawawekezaji wa kutosha, wengine wanaendelea na kazi za tafiti mbalimbali na wengine wako katika hatua ya kuanza uchimbaji wa makaa ya mawe,” amesema Mwalimu Maghembe.

spot_img

Latest articles

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

More like this

Wanawake TRA Wapongezwa kwa Mchango wa Ukusanyaji Mapato

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba, amewapongeza wanawake wa...

Mchungaji Kimaro: Miradi ya Familia Ndio Suluhisho la Ajira kwa Vijana

Na Mwandishi Wetu  MCHUNGAJI wa Kanisa la Kiinjiri Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama Dk....

Kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani: TRA Yakabidhi Vifaa Tiba Vyenye Thamani ya Milioni 40

Na Tatu Mohamed KUELEKEA maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanayoadhimishwa kila mwaka Machi 8,...