Warning: Array to string conversion in /home/themedia/domains/themediabrains.com/public_html/wp-includes/shortcodes.php on line 434
Array

Viongozi wa Serikali za vijiji wahimizwa kuweka uwazi walengwa wa TASAF

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema ni jukumu la Watendaji wa Serikali za Vijiji kuwatambua wananchi ambao wanastahili kuingizwa kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kupitia mikutano ya vijiji ili kuwepo na uwazi pamoja na kuondoa malalamiko kutoka kwa wananchi ambao wana vigezo vya kuingizwa.             

Kikwete ameyasema hayo wakati akizungumza na wananchi na walengwa wa TASAF wa Kata ya Masaki, Kijiji cha Kisanga Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kukagua utekelezaji wa miradi ya TASAF.

Kikwete amesema kuwa, kuna baadhi ya wananchi ambao wanastahili kuingizwa kwenye mradi wa TASAF wenye sifa na vigezo lakini kutokana na kutoitishwa mikutano ya kijiji hupelekea baadhi yao kukosa nafasi ya kuingizwa kwenye mradi huo, hivyo amewataka viongozi hao kuendesha mikutano ya mara kwa mara ili kuondoa malalamiko ambayo yanaweza kutokea.

Aidha, Kikwete amesisitiza wananchi kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwani amekuwa akijitahidi kuboresha maisha ya wananchi wake kwa maendeleo ya Taifa la Tanzania.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete anaendelea na ziara ya kikazi katika Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma, kutatua changamoto zinazowakabili watumishi hao pamoja na kukagua utekelezaji wa Miradi ya TASAF.

spot_img

Latest articles

ZOEZI LA UVUTAJI NYAYA AWAMU YA PILI ENEO LA KIKOMBO NA MKONZE KATIKA MRADI WA CHALINZE–DODOMA KUANZA KESHO

📌TANESCO yasema baadhi ya Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya...

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...

MHANDISI SWEDI: NANENANE NI FURSA YA KUIMARISHA SEKTA YA MADINI

Na Mwandishi Wetu KAIMU Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Aziza Swedi, amesema...

More like this

ZOEZI LA UVUTAJI NYAYA AWAMU YA PILI ENEO LA KIKOMBO NA MKONZE KATIKA MRADI WA CHALINZE–DODOMA KUANZA KESHO

📌TANESCO yasema baadhi ya Mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Magharibi, Kanda ya...

SOKO BUBU LA MADINI LAGUNDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

▪️Watuhumiwa 14 wakamatwa na tuhuma za utoroshaji madini ▪️Waigeuza nyumba ya kupanga kama soko ▪️Waziri Mavunde...

Msajili wa Hazina ateta na Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais...